-
Spika wa Bunge la Iran aghairisha safari yake ya Uturuki baada ya nchi hiyo kuivamia kijeshi Syria
Oct 10, 2019 04:21Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) ameghairisha safari aliyokuwa amepanga kufanya nchini Uturuki kufuatia hatua ya nchi hiyo ya kuivamia kijeshi ardhi ya Syria.
-
Rais Rouhani: Njama za Marekani za mashinikizo ya kiwango cha juu dhidi ya taifa la Iran zimefeli
Oct 09, 2019 10:27Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, njama za Marekani za mashinikizo ya kiwango cha juu dhidi ya taifa la Iran zimefeli na kwamba takwimu zote na moyo na utanashati wa taifa la Iran vinaonesha kuwa, kipindi cha mashinikizo ya kiwango cha juu kimeyoyoma.
-
Jarida la Newsweek: Trump ameogopa vitisho vya Rais Erdoğan wa Uturuki kuhusu Syria
Oct 08, 2019 23:03Jarida la Newsweek la Marekani limemnukuu mmoja wa viongozi wa serikali ya nchi hiyo akisema kuwa, Rais Donald Trump amesalimu amri mbele ya matakwa ya Rais Recep Tayyip Erdoğan wa Uturuki kuhusiana na Syria na kuyakubali bila ya pingamizi lolote.
-
Uturuki yaihakikishia Iran, mashambulizi yake Syria ni ya muda mfupi
Oct 08, 2019 04:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki amemhakikishia mwenzake wa Iran kwamba, mashambulizi ya jeshi la nchi hiyo huko kaskazini mwa Syria yaliyoanza Jumatatu usiku ni ya muda mfupi.
-
Uturuki kuanzisha vyuo vitatu kaskazini mwa Syria
Oct 06, 2019 23:07Vyombo vya habari vya Uturuki vimeripoti juu ya uamuzi wa serikali ya Rais Recep Tayyip Erdoğan wa nchi hiyo wa kuanzisha vyuo vitatu, huko kaskazini mwa Syria, chini ya usimamizi wa Chuo Kikuu cha Gaziantep cha Uturuki.
-
Al Muallem na Pedersen wasisitiza kupiga hatua mazungumzo ya kamati ya katiba ya Syria
Sep 23, 2019 23:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria na Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Syria wamechukunguza masuala yaliyosalia kuhusu uundaji wa kamati ya katiba, utaratibu na hatua zinazopaswa kuchukuliwa katika uwanja huo.
-
Taasisi ya Russia yafichua maovu ya "Kundi la Kofia Nyeupe nchini Syria"
Sep 22, 2019 23:18Taasisi isiyo ya kiserikali ya Russia kwa jina la the Fund for Research of Problems of Democracy imefichua kuwa, lengo kuu la kundi la kigaidi la "Kofia Nyeupe" huko Syria ni kuchapisha taarifa na habari za uwongo na zisizo sahihi dhidi ya serikali ya nchi hiyo na kuhusu hali ya mambo nchini.
-
Mousavi: Kupunguza Iran uwajibikaji wake katika JCPOA kunaendelea katika fremu ya makubaliano hayo ya kimataifa
Sep 16, 2019 09:05Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kuendelea Tehran kupunguza uwajibikaji wake katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA kunafanyika katika fremu ya makubaliano hayo ya kimataifa.
-
Rais Bashar al-Assad wa Syria atoa amri ya msamaha kwa wote
Sep 16, 2019 03:36Rais Bashar al-Assad wa Syria ametoa amri ya msamaha kwa watuhumiwa ambao hawakufanya jinai kama za kuua watu nchini humo.
-
Kutambuliwa kimataifa kwamba mashambulizi ya Marekani nchini Syria ni jinai ya kivita
Sep 12, 2019 05:55Muungano wa kimataifa wa eti kupambana na Daesh (ISIS) unaoongozwa na Marekani uliundwa mwaka 2014 kwa madai ya kukabiliana na genge hilo la kigaidi, na umekuwa ukifanya mashambulizi ya kiholela nchini Syria bila ya kuwa na taathira zozote za maana mbaya kwa genge hilo la ukufurishaji.