-
China yaonya, tutatoa jibu Rais wa Taiwan akikutana na Spika wa US
Mar 30, 2023 02:15China imeionya vikali Washington na kusisitiza kuwa itachukua 'hatua ya kujibu mapigo' iwapo Rais wa Taiwan, Tsai Ing-wen atakutana na Spika wa Kongresi ya Marekani, Kevin McCarthy katika safari yake inayotazamiwa kufanyika karibuni.
-
China yalalamikia safari za maafisa wa Ujerumani na Uingereza huko Taiwan
Mar 23, 2023 06:56Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya China imelalamikia vikali safari ya Bettina Stark-Wattsinger, Waziri wa Elimu wa Ujerumani katika Kisiwa cha Taiwan na kusisitiza kuwa inapinga safari rasmi ya waziri huyo katika kisiwa hicho kinachomilikiwa na serikali ya Beijing.
-
Marekani yapiga ngoma ya vita kwa kuipa Taiwan 'msaada' wa kijeshi
Sep 16, 2022 04:02Bunge la Seneti la Marekani limepasisha muswada wa sheria inayotaka Taiwan kupewa msaada wa kijeshi wa mabilioni ya dola, hatua inayotazamiwa kuighadhabisha China.
-
Marekani kuiwekea vikwazo China ili 'kuzuia' kuvamiwa Taiwan
Sep 14, 2022 07:34Marekani imeripotiwa kuwa inatafakari kuiwekea China vikwazo ili kuzuia eti mashambulizi tarajiwa ya kijeshi ya Beijing dhidi ya kisiwa cha Taiwan.
-
Onyo la China kwa Canada kuhusu safari ya wabunge wake Taiwan
Aug 26, 2022 02:25China imeionya vikali Canada na kusisitiza kuwa itachukua hatua madhubuti na za nguvu iwapo wabunge wa Canada watafanya safari ya kuitembelea Taiwan karibuni hivi.
-
Kiwewe cha Marekani kwa kuzidi kuongezeka nguvu za China
Aug 20, 2022 02:41Marekani ambayo imeingia kiwewe kutokana na kuzidi kuongezeka nguvu za China, imeahidi kuchukua hatua za kukabiliana na Beijing katika kipindi cha wiki na miezi ijayo karibu na kisiwa cha Taiwan, kwa tamaa ya kupunguza kasi ya nguvu za kijeshi na kiuchumi za China.
-
China: Uhuru wa Taiwan maana yake ni vita
Aug 19, 2022 04:04Balozi wa China mjini London ameonya kuwa, uingiliaji wa mambo unaofanywa na Uingereza na Marekani juu ya suala la Taiwan hautakuwa na matokeo mengine ghairi ya vita.
-
Bloomberg: China ina uwezo wa kuteketeza kwa muda mfupi ndege 900 za kivita za Marekani
Aug 13, 2022 01:31Jarida la Bloomberg linalochapishwa Marekani limeandika kuwa, endapo vitazuka vita baina ya Marekani na China kwa sababu ya Taiwan, Wachina wataweza kwa muda mfupi kuziangamiza ndege za kivita 900 za Marekani, yaani nusu ya uwezo wote wa kikosi cha anga cha nchi hiyo.
-
Onyo la jeshi la China kwa chokochoko za Taiwan
Aug 12, 2022 06:36Jeshi la China limekionya kisiwa cha Taiwan dhidi ya kuendeleza chokochoko katika eneo hilo la kistratijia.
-
Taiwan yadai kuwa China inataka kuivamia kijeshi
Aug 10, 2022 01:21Taipei imedai kuwa China inapanga njama ya kukivamia kisiwa cha Taiwan, baada ya Beijing kutangaza duru mpya ya mazoezi ya kijeshi katika maji ya kisiwa hicho, ukiwa ni muendelezo wa kujibu mapigo kwa ziara iliyofanywa na Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani, Nancy Pelosi katika kisiwa hicho hivi karibuni.