-
Zitto Kabwe: Mungu aliamua niingie mahabusu ili nijionee mateso wanayopata wananchi wenzangu Tanzania
Feb 23, 2018 11:48Mbunge wa jimbo la Kigoma Mjini, magharibi mwa Tanzania kupitia chama cha ACT- Wazalendo, Zitto Zuberi Kabwe amesema kuwa, inawezekana Mungu aliamua yeye akamatwe jana na polisi na kisha apelekwe mahabusu ili aweze kushuhudia mateso wanayoyapata watu wanaozuiliwa korokoroni kinyume cha sheria.
-
Viongozi wa dini na wanasiasa wapanga kuonana na Rais Magufuli wa Tanzania
Feb 22, 2018 04:42Viongozi wa dini na wanasiasa nchini Tanzania wamekusudia kwenda kumuona Rais John Magufuli wa nchi hiyo kwa ajili ya kuwasilisha pendekezo la kutaka kukamilishwa mchakato wa kupatikana Katiba Mpya.
-
Hali ya kisiasa nchini Tanzania na wito wa asasi za kiraia wa kuundwa tume ya uchunguzi
Feb 22, 2018 04:15Licha ya serikali ya awamu ya tano ya Tanzania chini ya Rais John Pombe Magufuli kusifika kwa mapambano yake dhidi ya ufisadi na pia kulinda raslimali ya nchi hiyo, lakini imekuwa ikikosolewa na wapinzani kutokana na miamala yake kuvilenga vyama vya upinzani nchini.
-
Asasi za kiraia Tanzania zataka kuundwa tume ya kuchunguza mauaji
Feb 21, 2018 11:51Makundi ya kiraia nchini Tanzania yametoa wito wa kuundwa tume huru ya kuchunguza vifo ambavyo vimekuwa vikitokea nchini humo katika mazingira ya kutatanisha hasa katika siku za hivi karibuni.
-
CCM yatwaa majimbo ya Kinondoni na Siha, askari 6 wakamatwa mauaji ya mwanachuo
Feb 18, 2018 12:15Chama cha Mapinduzi (CCM) huko nchini Tanzania kimetangazwa mshindi wa chaguzi ndogo za majimbo ya Siha mkoani Kilimanjaro na Kinondoni jijini Dar es Salaam ambayo kabla ya kujiuzulu wabunge wake yalikuwa mikononi mwa vyama vya upinzani.
-
Uchaguzi mdogo Tanzania wagubikwa na machafuko; CCM yaelekea kushinda
Feb 17, 2018 13:47Polisi nchini Tanzania imethibitisha kuwa mtu mmoja ameuawa kwa kupigwa risasi na polisi katika vurugu zilizohusiana na uchaguzi mdogo wa bunge uliofanyika leo katika jimbo la Kinondoni lililoko katika mji mkuu wa Tanzania, Dar es Salaam.
-
Chaguzi ndogo zenye mchuano mkali zafanyika Tanzania
Feb 17, 2018 05:21Habari kutoka nchini Tanzania zinasema kuwa zoezi kupiga kura katika chaguzi ndogo za ubunge na udiwani katika baadhi ya maeneo, Tanzania Bara limeanza rasmi asubuhi ya leo Jumamosi tarehe Februari 17, 2018.
-
Tanzania yamkabidhi kiongozi wa waasi wa Kongo DR kwa serikali ya nchi hiyo
Feb 05, 2018 13:08John Tshibangu, Kanali mwasi wa jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo aliyetishia kumuondoa madarakani rais wa nchi hiyo Joseph Kabila amehamishwa kutoka Tanzania na kukabidhiwa kwa serikali ya DRC ambako atashtakiwa kwa kufanya uasi.
-
Jitihada za Kudhibiti Homa ya Chikungunya Kenya na Tanzania
Jan 20, 2018 03:59Serikali Kenya na Tanzania ziko mbioni kudhibiti ugonjwa wa Homa ya Chikungunya ambao huambukizwa na mbu aina ya aedes na hauna tiba mahsusi wala kinga.
-
Sakata la meli zinazobeba mihadarati zikiwa na bendera ya TZ, lamlazimu Rais Magufuli kusitisha usajili wa meli
Jan 20, 2018 01:16Rais John Pombe Magufuli wa Tanzania ameagiza kusitishwa mara moja usajili wa meli mpya nchini humo kufuatia kukamatwa dawa za kulevya na bidhaa nyingine zilizopigwa marufuku kimataifa ndani ya meli zinazopeperusha bendera ya Tanzania.