-
Abu Hatab wa Ghaza asimulia alivyoshiriki kuzika Wapalestina 18,000 waliouliwa kinyama na Israel
Dec 23, 2025 12:02Mzikamaiti Yousef Abu Hatab mkazi wa Ukanda wa Ghaza na mmoja wa mashuhuda wa moja ya majanga makubwa zaidi kuwahi kutokea katika historia ya Palestina, amesema ameshiriki kuzika karibu miili 18,000 ya Wapalestina waliouliwa shahidi wakati wa vita vya kinyama na vya mauaji ya kimbari yaliyofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel katika eneo hilo la Palestina.
-
Wademocrat wataka kushinikizwa Israel kwa kukiuka usitishaji vita Gaza
Dec 23, 2025 08:00Makumi ya Wademokrat katika Bunge la Marekani wameitaka Ikulu ya Rais wa nchi hiyo (White House) kuushinikiza kidiplomasia utawala wa Israel ili usitishe ukiukaji wa mapatano ya kutisha mapigano katika Ukanda wa Gaza.
-
Baridi kali yaua Wapalestina 17 Gaza; Israel yaendelea kuzuia misaada
Dec 18, 2025 10:26Dhoruba na baridi kali zimesababisha vifo vya Wapalestina 17 katika Ukanda wa Gaza tangu mwanzoni mwa mwezi huu, kwa mujibu wa serikali za mitaa Gaza, huku Israel ikishadidisha vikwazo vikali vya kuingia kwa vifaa vya kuunda makazi na misaada mingine ya kibinadamu katika eneo hilo la Palestina lililokumbwa na vita.
-
Qatar: Ukiukaji wa usitishaji mapigano wa Israel 'unahatarisha' mchakato mzima wa Gaza
Dec 18, 2025 10:25Waziri Mkuu wa Qatar ameonya kwamba, ukiukaji unaofanywa kila siku wa Israel wa makubaliano ya kusitisha mapigano Gaza unatishia mchakato mzima wa mapatano hayo, huku akitoa wito wa kutekelezwa haraka awamu inayofuata ya makubaliano hayo ili kukomesha vita vya mauaji ya halaiki vya Israeli dhidi ya eneo la Wapalestina lililozingirwa.
-
Albanese: Israel na waungaji mkono wake wakuu inawapasa wagharamie ujenzi mpya wa Ghaza
Dec 13, 2025 11:36Francesca Albanese, Ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu amesema, Israel na Marekani pamoja na nchi zingine ambazo zilikuwa wasambazaji wakuu wa silaha kwa utawala huo, zinapaswa kugharimia ujenzi mpya wa eneo la Ukanda wa Ghaza.
-
Ripoti: US inaishinikiza Israel iuondoe mlima wa kifusi uliozagaa Ghaza baada ya miaka 2 ya vita
Dec 12, 2025 10:10Marekani imeitaka Israel ibebe jukumu la kuondoa vifusi vikubwa vilivyotapakaa kwenye kila pembe ya Ukanda wa Ghaza baada ya zaidi ya miaka miwili ya vita vya kinyama na mauaji ya kimbari iliyofanya dhidi ya Wapalestina wa eneo hilo, pamoja na uharibifu mkubwa uliosababishwa na mashambulizi yake ya anga na matingatinga ya kivita. Hayo yameelezwa na toleo la Alkhamisi la gazeti la kizayuni la Yedioth Ahronoth.
-
HAMAS: Tuko tayari kukabidhi silaha kwa utawala wa Wapalestina ikiwa Israel itaondoka kikamilifu Ghaza
Dec 08, 2025 02:34Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema, iko tayari kukabidhi silaha zake katika Ukanda wa Ghaza kwa mamlaka ya utawala ya Wapalestina itakayosimamia uendeshaji wa eneo hilo, kwa sharti kwamba uvamizi na ukaliaji ardhi kwa mabavu wa jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel ukomeshwe kikamilifu.
-
Yasser Abu Shabab, mshirika wa Israel na msaliti wa Wapalestina wa Ghaza aripotiwa kuuawa
Dec 05, 2025 06:55Yasser Abu Shabab, mshirika wa kijeshi wa utawala wa kizayuni wa Israel mwenye uhusiano pia na kundi la kigaidi la DAESH (ISIS), maarufu kwa kuongoza uporaji wa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza na kwa kuwalenga kwa kuwaua raia wa Palestina, ameripotiwa kuuawa katika eneo hilo.
-
Amnesty International: Israel inaendelea kufanya mauaji ya kimbari Ghaza
Nov 29, 2025 11:14Shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limetangaza kuwa, utawala wa kizayuni wa Israel "unaendelea bila kusita kufanya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina huko Ghaza, licha ya usitishaji mapigano" ulioanza kutekelezwa tarehe 10 Oktoba.
-
Baada ya Israel kuwaua Wapalestina wengine 24 Ghaza, HAMAS yataka wapatanishi, hasa US iingilie kati
Nov 23, 2025 07:05Jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel limefanya mashambulizi makali ya anga katika maeneo tofauti ya Ukanda wa Ghaza, na kuwaua shahidi Wapalestina wasiopungua 24, wakiwemo watoto, katika mwendelezo wa ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa tangu wiki sita zilizopita kwenye eneo hilo la Palestina lililoteketezwa kwa vita.