-
White House: Trump atakutana na viongozi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu kujadili kadhia ya Ghaza
Sep 23, 2025 06:57Msemaji wa ikulu ya White House Karoline Leavitt ametangaza kuwa rais wa Marekani Donald Trump anatazamiwa kufanya mkutano na viongozi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu kujadili kadhia ya Ghaza.
-
Jihadul-Islami: US na Magharibi hazitaki vita Ghaza vikomeshwe mpaka makundi yote ya Muqawama yaangamizwe
Sep 23, 2025 06:30Harakati ya Jihadul-Islami ya Palestina imesema, hakuna mapendekezo mapya ya kusitisha vita Ghaza ambayo yamepokelewa hadi sasa na kuongeza kuwa, Marekani na nchi za Magharibi hazitaki kukomesha vita hivyo hadi pale makundi yote ya Muqawama yanayoupinga utawala wa kizayuni wa Israel, -na si Palestina pekee- bali katika eneo lote, yatakapotokomezwa.
-
Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa: Hali ya Ghaza haikubaliki, vita lazima vikome
Sep 23, 2025 06:30Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Annalena Baerbock ameuambia mkutano wa suluhisho la mataifa mawili uliofanyika makao makuu ya umoja huo jana Jumatatu: "nchi-dola huru ya Palestina lazima ianzishwe".
-
Marekani inatafakari kuiwekea vikwazo mahakama nzima ya ICC kwa kuchunguza jinai za Israel Ghaza
Sep 23, 2025 06:29Marekani inatafakari juu ya kuiwekea vikwazo vikali Mahakama nzima ya Kimataifa ya Jinai (ICC) mapema wiki hii, hatua ambayo inaweza kuvuruga sana shughuli za mahakama hiyo katika kuchunguza uhalifu wa kivita uliofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel huko Ghaza.
-
Askari wanne wa utawala wa kizayuni waangamizwa, wanane wajeruhiwa kusini mwa Ghaza
Sep 18, 2025 10:42Vyanzo vya habari vimeripoti kuwa wanajeshi wanne wa utawala wa kizayuni wa Israel wameangamizwa na wengine wanane wamejeruhiwa katika mripuko wa bomu lililotegwa ardhini kusini mwa Ukanda wa Ghaza.
-
Israel yashadidisha mauaji dhidi ya wakazi wa Gaza; mashinikizo ya kimataifa yaongezeka dhidi yake
Sep 18, 2025 07:23Idadi ya vifo vya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza inaendelea kuongezeka huku mashambulizi ya kijeshi na mauaji ya kimbari ya Israel yakiingia mwaka wa pili sasa, na hivyo kuzidisha ukosoaji kimataifa.
-
Wabunge wa UK: Vikosi vya kijeshi vitakavyoongozwa na UN vipelekwe Ghaza kuzuia mauaji ya kimbari
Sep 18, 2025 03:46Wabunge watano wa Uingereza wamemwandikia barua waziri wao wa mambo ya nje Yvette Cooper wakiitaka serikali ya London "ifuatilie kwa dharura uingiliaji kati wa kijeshi utakaoongozwa na Umoja wa Mataifa" ili kukomesha mauaji ya kimbari ya yanayofanywa na Israel huko Ghaza.
-
Israel yashambulia kwa mabomu mnara wa 50 wa makazi katika mji wa Gaza
Sep 08, 2025 07:33Utawala wa Israel umeshadidisha mashambulizi yake ya kinyama katika Ukanda wa Gaza kwa kushambulia na kubomoa jengo jingine la mnara wa 50 wa makazi ya Wapalestina katika mji wa Gaza huku ikitekeleza mashambulizi ya nchi kavu kwa lengo la kulikalia kwa mabavu eneo hilo.
-
Jeshi la kizayuni laporomosha jengo la ghorofa 12 linalowapa hifadhi mamia ya Wapalestina Ghaza
Sep 06, 2025 03:06Jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel siku ya Ijumaa liliripua na kuporomosha jengo la ghorofa 12 la makazi ya raia magharibi mwa Mji wa Ghaza linalowapa hifadhi mamia ya Wapalestina waliolazimika kuyahama makazi yao katika eneo hilo lenye msongamano wa watu na ambalo limekuwa kimbilio la makumi ya maelfu ya Wapalestina.
-
IRIB yalaani mauaji ya mwanahabari wa Al-Alam huko Gaza
Sep 03, 2025 06:27Kitengo cha Kimataifa cha Shirika la Utangazaji wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran IRIB kimelaani vikali mauaji ya Rasmi Jihad Salem, mpigapicha wa kanali yake ya Kiarabu ya Al-Alam, ambaye aliuawa shahidi katika shambulio la Israel huko Gaza jana Jumanne, Septemba 2 alipokuwa akirejea kutoka kazini.