-
Ripoti: Israel iliwamiminia risasi, kuwaua wafanyakazi wa misaada Tel al Sultan, Gaza
Feb 25, 2026 02:26Karibu risasi elfu moja zilifyatuliwa na wanajeshi wa Israel katika mauaji ya kiholela dhidi ya wafanyakazi wa misaada huko Tel al-Sultan, Gaza, huku baadhi yao wakiuawa kwa kupigwa risasi kwa karibu, kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa hivi karibuni.
-
Israel imepeleka Ghaza maboksi yenye mafuvu na miili iliyonyofolewa ya wanawake Wapalestina
Feb 24, 2026 11:15Mbunge wa kujitegemea, ambaye pia ni kiongozi wa zamani wa chama cha Leba nchini Uingereza Jeremy Corbyn, ametoa simulizi za kutisha zilizotokana na maelezo ya mkurugenzi wa Hospitali ya Al-Shifa katika Ukanda wa Ghaza uliozingirwa, zinazobainisha kwa undani jinsi utawala wa kizayuni wa Israel ulivyopeleka katika eneo hilo masanduku kadhaa yenye mafuvu ya vichwa na mabaki ya Wapalestina yaliyokatwakatwa.
-
Hamas yalaani mkutano wa 'Bodi ya Amani' ya Trump
Feb 20, 2026 09:48Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imelaani vikali kufanyika mkutano wa kile kinachoitwa 'Bodi ya Amani ya Gaza' huko nchini Marekani.
-
Waholanzi 640 waliohudumu katika jeshi la Israel Gaza kushtakiwa?
Feb 20, 2026 03:26Zaidi ya raia 640 wa Uholanzi wamehudumu katika jeshi la Israel wakati wa vita vya mauaji ya halaiki vya utawala huo wa Kizayuni dhidi ya Gaza na kwneye mashambulizi dhidi ya Ukingo wa Magharibi, takwimu mpya zinaonyesha, huku wataalamu wa sheria wakionya kwamba, wale waliohusika wanaweza kushtakiwa chini ya sheria za kimataifa na za nchi hiyo za uhalifu wa kivita.
-
Zaidi ya raia 2,000 wa UK wamepigana kwa niaba ya Israel katika mauaji ya halaiki Gaza
Feb 13, 2026 02:02Maelfu ya raia wa Uingereza wamehudumu katika jeshi la Israel wakati wa vita vya mauaji ya halaiki vya utawala huo wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Akademia ya Geneva: Waliofariki Ghaza wanakaribia 200,000, watu wamepungua kwa 10%
Feb 08, 2026 02:26Stuart Casey Maslen, mkuu wa Akademia ya Geneva ya Sheria za Kimataifa za Kibinadamu na Haki za Binadamu amesema, tangu Oktoba 2023 hadi sasa, idadi ya watu huko Ghaza imepungua kwa zaidi ya 10%, hali inayoashiria kutokea vifo takribani laki mbili.
-
Guardiola apaza sauti tena kuhusu mauaji ya kimbari ya Ghaza na dhulma inayotawala duniani
Feb 05, 2026 06:05Kocha wa timu ya soka ya Manchester City, Pep Guardiola, amesema mauaji ya watu wasio na hatia duniani kote yanamuathiri sana na amewahimiza walimwengu wasinyamazie kimya dhulma zinazofanywa.
-
Israel yaendelea kumwaga damu za Wapalestina, yaua 20 Gaza
Feb 04, 2026 10:23Mashambulizi mapya ya kinyama ya utawala wa Kizayuni wa Israel yamewaua shahidi watu wasiopungua 20, wakiwemo watoto wadogo katika Ukanda wa Gaza.
-
Israel yaua Wapalestina 31 wakiwemo watoto 6 katika ukiukaji mpya wa usitishaji vita Ghaza
Jan 31, 2026 14:44Wapalestina wasiopungua 31, wakiwemo kwa uchache watoto sita, wameuawa shahidi katika mashambulizi ya kinyama yaliyofanywa na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel tangu alfajiri ya leo hadi wakati huu katika Jiji la Ghaza na mji wa Khan Younis katika Ukanda wa Ghaza.
-
Katika mazungumzo na US, Misri yahimiza Israel iondoke Ghaza, ifungue tena kivuko cha Rafah
Jan 26, 2026 03:50Waziri wa Mambo ya Nje wa Misri Badr Abdelatty ametoa wito kwa utawala wa kizayuni wa Israel kujiondoa katika Ukanda wa Ghaza na kufungua tena kivuko cha mpakani cha Rafah kuliingana na makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyoanza kutekelezwa Oktoba mwaka jana.