Wizara ya Ulinzi ya Russia imetangaza kuwa imezidhibiti na kuzitungua ndege kadhaa zisizo na rubani za Ukraine (Droni) katika Peninsula ya Crimea.
Mkuu wa Idara ya Intelijensia ya Jeshi la Ukraine amekadhibisha uvumi kwamba Iran imeiuzia Russia makombora ya balestiki kwa ajili ya kutumika katika vita vya Ukraine.
Matokeo ya uchunguzi wa karibuni kabisa wa maoni yanaonesha kuwa, ni asilimia 10 tu ya wananchi wa nchi za Ulaya wanaoamini kwamba Ukraine inaweza kushinda kwenye vita vyake na Russia.
Rais wa zamani wa Russia Dmitry Medvedev ametishia Washington, Berlin, London na Kiev kushambuliwa kwa silaha za nyuklia ikiwa Russia italazimishwa kujiondoa Ukraine.
Rais wa Russia amesema kuwa Moscow iko tayari kumaliza vita na Kiev kwa amani, lakini hakuna dalili kwamba Ukraine inataka amani.
Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) imepinga takriban tuhuma zote zilizowasilishwa na Ukraine katika kesi ya kufadhili ugaidi dhidi ya Russia.
Rais wa Ukraine amekiri kuwa jeshi la nchi hiyo ni dhaifu mkabala wa Russia na kusema: Ulaya peke yake haiwezi kuisaidia Ukraine dhidi ya Russia bila uungaji mkono wa Marekani.
Umoja wa Ulaya umelazimika kubeba zigo zito la madeni kutokana na kuifuata kibubusa Marekani katika kuiunga mkono Ukraine kwenye vita na Russia.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema kuwa Marekani inaona vita kati ya Russia na Ukraine kama "mradi wa faida" na kusema: Moscow iko tayari kwa mazungumzo na Ukraine kwa ajili ya kumaliza mzozo huo.
Mkuu wa Shirika la Intelijensia la Russia amesema, Marekani imeanza kuunda "serikali ya kikoloni" nchini Ukraine inayojumuisha wanasiasa wa ndani ambao wamekula kiapo cha utiifu kwa Washington.