-
Indhari ya UN kuhusiana na kushamiri ubaguzi na uenezaji chuki ndani ya jamii ya Marekani
Nov 25, 2021 23:17Fernand de Varennes, ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya haki za binadamu za jamii za wachache, ametahadharisha juu ya kuzidi kupanuka ufa wa kukosekana usawa na uenezaji chuki dhidi ya jamii za wachache katika mfumo wa vyombo vya mahakama na vyombo vya habari vya Marekani na kutilia mkazo udharura wa kuanzishwa sheria ya kimataifa ya kukabiliana na uenezaji chuki.
-
Msemaji wa UN: Mfumo wa fedha na kibenki wa Afghanistan unakaribia kusambaratika
Nov 23, 2021 08:38Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa mara nyingine ametahadharisha kuhusu mgogoro wa kiuchumi huko Afghanistan na kueleza kuwa mfumo wa fedha na kibenki wa nchi hiyo unakaribia kuanguka.
-
Iran yataja sababu ya kuenea uhalifu na ugaidi kote duniani
Nov 23, 2021 00:00Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema sababu kuu ya kuenea uhalifu na ugaidi katika maeneo mbalimbali ya dunia ni magendo na biashara haramu ya silaha nyepesi na ndogo.
-
Umoja wa Mataifa watoa wito wa kuhitimishwa vita kaskazini mwa Ethiopia
Nov 20, 2021 04:45Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito wa kuhitimishwa vita na mapigano kati ya serikali ya Ethiopia na wapiganaji wa Harakati ya Ukombozi ya Watu wa Tigray (TPLF) kaskazinii mwa nchi hiyo.
-
UN: Mauaji ya waandamanaji Sudan ni ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu
Nov 19, 2021 08:09Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa amelaani vikali mauaji ya watu 39 nchini Sudan yaliyofanywa na vikosi vya ulinzi tangu yalipofanyika mapinduzi ya kijeshi nchini humo tarehe 25 Oktoba mwaka huu.
-
UN: Waliohusika na mauaji ya mateka 10 wa kivita Yemen wafunguliwe mashtaka
Nov 18, 2021 23:26Msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa taarifa akilaani mauaji yaliyofanywa na mamluki na vibaraka wa Saudi Arabia dhidi ya matekani 10 wa vita wa jeshi la Yemen na kusema kuwa mauaji hayo yanakiuka sheria za kimataifa na haki za binadamu.
-
UNICEF: Watoto wana imani na mustakabali bora duniani kuliko watu wazima
Nov 18, 2021 04:29Kura ya maoni iliyoendeshwa katika nchi 21 ikihusisha watoto na watu wazima imeonesha kuwa watoto wanaamini dunia inakuwa bora zaidi huku watu wazima wakiwa na shaka na shuku.
-
UN yatiwa wasiwasi na kukamatwa maelfu ya Watigray katika mji mkuu wa Ethiopia
Nov 16, 2021 23:31Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za bindamu, OHCHR, imeelezea wasiwasi wake kufuatia vitendo vya ukamataji wa watu vilivyofanyika wiki iliyopita katika mji mkuu wa Ethiopia, Addis Ababa, na pia katika maeneo ya Gondar, Bahir Dar na mengineyo, huku polisi wakitumia vifungu vingi vya hali ya hatari iliyotangazwa tarehe 2 Novemba ili kuwatafuta, kuwakamata na kuwaweka watu kizuizini.
-
Umoja wa Mataifa wakosoa vitendo vya mabavu vya nchi za Ulaya dhidi ya wakimbizi
Nov 13, 2021 08:19Akizungumza katika bunge la Ulaya Filippo Grandi Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR amekosoa vitendo vya mabavu na ukandamizaji wa Umoja wa Ulaya dhidi ya wakimbizi na kusisitiza kuwa siku zote na mara kwa mara tunashuhudia raia wanaotafuta hifadhi barani Ulaya wakifukuzwa kwa mabavu na visingizio vya kisheria kutumika katika kuwanyima hifadhi raia hao.
-
Umoja wa Mataifa waonya kuhusu mgogoro wa kibinadamu nchini Afghanistan
Nov 13, 2021 00:48Mwakilishi wa Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini Afghanistan ametahadharisha kuhusu mgogoro mkubwa wa kibinadamu unaoinyemelea nchi hiyo.