-
Indhari ya Josep Borrell kwa Israel kuhusu kuendelea kuzikalia kwa mabavu ardhi za Palestina
May 19, 2020 22:39Katika fremu ya malengo yake ya muda mrefu, utawala haramu wa Israel unakusudia kupora sehemu kubwa ya ardhi za Palestina za Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kuziunganisha na ardhi nyingine za Palestina unazozikali kwa mabavu.
-
Borrell: EU haitaitambua hatua ya upande mmoja ya Israel ya kuambatisha ardhi inayoikalia kwa mabavu
May 19, 2020 10:57Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya ameuonya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel dhidi ya utekelezaji wa uamuzi wa "upande mmoja" wa kuambatisha na kile kinachoitwa Israel baadhi ya sehemu za ardhi ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu akisisitiza kuwa jumuiya hiyo yenye nchi wanachama 27 haitayatambua mabadiliko yoyote ya aina hiyo yanayokinzana na muundo wa mipaka ya mwaka 1967.
-
Wanadiplomasia wa EU: Marekani haina haki ya kutaka kurefushwa vikwazo vya silaha dhidi ya Iran
May 06, 2020 03:31Wanadiplomasia wa Umoja wa Ulaya wamesema kwa kujiondoa kwenye makubaliano ya nyuklia ya Iran, Marekani ilipoteza haki yake ya kutaka kurefushwa vikwazo vya silaha vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Iran.
-
Msimamo mmoja wa dunia dhidi ya mpango wa utawala wa Kizayuni na uungaji mkono wa Marekani kwa mpango huo
Apr 26, 2020 20:10Serikali ya Rais Donald Trump imekuwa ikichukua hatua zisizo za kawaida katika kuunga mkono utawala haramu wa Kizayuni ambapo kati ya hatua hizo ni kuafiki rasmi suala la kuunganishwa maeneo ya Ukingo wa Magharibi na maeneo mengine yanayokaliwa kwa mabavu na utawala huo bandia.
-
Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa Libya yapinga mpango wa EU wa kuzuia kuingizwa silaha nchini humo
Apr 25, 2020 08:43Vita vya ndani nchini Libya vilivyoanza baada ya kung'olewa madarakati dikteta wa zamani wa nchi hiyo, Muammar Gaddafi vimeshika mwelekeo unaotia wasiwasi mkubwa zaidi tangu Aprili mwaka jana 2019 kufuatilia mashambulizi ya wapiganaji wa linalojiita jeshi la taifa la Libya chini ya uongozi wa Khalifa Haftar, lengo likiwa ni kuudhibiti mji mkuu, Tripoli na kuing'oa madarakani Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa.
-
Mtihani wa Corona na sisitizo la Italia la kutokuwepo mshikamano ndani ya Umoja wa Ulaya
Apr 22, 2020 05:47Kuenea kwa kiasi kikubwa virusi vya Corona barani Ulaya na mgogoro unaotokana na janga hilo, kumezifanya nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya EU kukosoa baadhi ya sheria zake na kusema kuwa haujakuwa na radiamali wala kuonyesha mshikamano uliotarajiwa kuhusiana na janga hilo.
-
Baada ya janga la corona Wataliano wataka kujiondoa Umoja wa Ulaya
Apr 20, 2020 03:30Uchunguzi mpya wa maoni nchini Italia umebaini kuwa aghalabu ya watu wa nchi hiyo wanataka nchi yao iondoke katika Umoja wa Ulaya kutokana na utendaji mbovu wa umoja huo katika kipindi hiki cha janga la corona nchini humo.
-
Tahadhari ya maafisa wa Italia kuhusu uwezekano wa kusambaratika EU
Apr 14, 2020 01:59Maambukizi ya virusi vya corona na kutokuwepo ushirikiano kwa ajili ya kudhibiti kasi ya maambukizi ya virusi hivyo katika nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya (EU) vimetia mashakani mustakbali wa umoja huo na malengo ya kuasisiwa kwake.
-
Jitihada za Umoja wa Ulaya za kulinda mshikamano na uchumi wa pamoja
Apr 12, 2020 03:06Kutokana na kuendelea janga la ugonjwa wa corona barani Ulaya na kuongezeka wasiwasi kuhusu taathira mbaya za kiuchumi na kisiasa kutokana na janga hilo, wakuu wa Umoja wa Ulaya wametenga mfuko wa dharura wa Euro billioni 500 kwa ajili ya kukabiliana na madhara yanayotokana na ugonjwa huo angamizi.
-
Iran kurutubisha urani hadi SWU milioni moja iwapo EU itafeli kutoa dhamana ya kutekeleza JCPOA
Apr 09, 2020 03:52Kamati ya Usalama wa Taifa na Sera za Kigeni ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) imesema Tehran itaendelea kurutubisha urani kwa kiwango inachotaka, lakini inaweza kuangalia upya urutubishaji huo iwapo tu Umoja wa Ulaya utatoa dhamana ya kivitendo ya kuheshimu na kufungamana na makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.