Katika ziara yake nchini China, Waziri Mkuu wa Russia amesema kuimarishwa uhusiano wa pande mbili ni kwa manufaa ya Moscow na Beijing.
Ivan Khel Pinto, Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela amesema katika mahojiano aliyofanyiwa na televisheni ya Al Mayadeen kwamba, uhusiano mzuri wa nchi yake na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni wa muda mrefu, ni wa jadi na ni mkubwa.
Balozi wa Afrika Kusini nchini Iran amekosoa kuendelea vikwazo vya madola ya Magharibi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Jumapili ya jana tarehe 27 Februari, Brigedia Jenerali Hamid Vahedi, Kamanda wa Kikosi cha Anga cha Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran aliwasili katika mji mkuu wa Pakistan Islamabad kwa minajili ya kukutana na kufanya mazungumzo na maafisa wa kijeshi na kisiasa wa nchi hiyo.
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, irada ya kisiasa ya serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ni kukuza na kustawisha ushirikiano na mataifa rafiki hususan Oman.
Zamir Kabulov, mjumbe wa Rais wa Russia katika masuala ya Afghanistan amesema katika mkutano wa Valdai Discussion Club kwamba: Askari wa Marekani na waitifaki wake walikuwa na mawasiliano na ushirikiano na kundi la kigaidi la Daesh nchini Afghanistan.
Msemaji wa White House ametoa radiamali yake kufuatia kusainiwa mpango wa ushirikiano wa kimkakati wa miaka 25 kati ya Iran na China.
Kwa mujibu wa azimio nambari 2231 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa vikwazo vya silaha vya Iran vinamalizika tarehe 18 mwezi huu wa Oktoba 2020 baada ya kumalizika muda wa miaka mitano wa vikwazo hivyo. Russia ikiwa mwanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama na moja kati ya nchi wanachama wa kundi la 4+1 imesisitiza kwamba itashirikiana kijeshi na Iran baada ya kumalizika vikwazo licha ya Marekani kufanya juhudi za kuongeza muda wa vikwazo hivyo.
Rais Nicolas Maduro wa Venezuela ameishukuru Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa msaada wake kwa nchi hiyo katika kukabiliana na vikwazo vya mafuta vya Marekani dhidi ya Venezuela na kusisitiza kuwa, uzoefu wa Iran utaweza kuisaidia nchi yake kutia nguvu uwezo wake wake wa kujitawala.
Katika miaka ya hivi karibuni Iran na Venezuela zimeandamwa na vikwazo vya kiuchumi na kisiasa vya Marekani na viongozi wa White House wamefanya juhudi kubwa kutumia nyenzo mbalimbali ili wazifanye nchi mbili hizi zisalimu amri na kufuata siasa za Washington.