Feb 26, 2016 16:20
Matukio yanayojiri nchini Bahrain yanaonyesha kuwa utawala wa Aal Khalifa unazidisha hatua za ukandamizaji dhidi ya wananchi kiasi kwamba kuwatia nguvuni na kuwafungulia kesi wanaharakati wa kisiasa kunazidi kuchukua sura pana zaidi inayozidi kutia wasiwasi siku baada ya siku.