-
Katika wiki moja vifo 18, maambukizi 1,300 ya kipindupindu yaripotiwa Sudan iliyogubikwa na vita
Jul 23, 2025 02:42Wizara ya Afya ya Sudan imeripoti maambukizi mapya ya kipindupindu, huku idadi hiyo ikifika 1,307 na vifo 18 vilivyosababishwa na ugonjwa huo ndani ya muda wa wiki moja.
-
Mkuu wa Sera za Nje wa EU: Machaguo yote dhidi ya Israel yako mezani
Jul 23, 2025 00:10Kaja Kallas, Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya ametuma ujumbe katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X akisema: Mauaji ya watu wasio na ulinzi wa Palestina yanapasa kusitishwa; vinginevyo machaguo yote yako mezani.
-
Wanajeshi wa Israel wawauwa shahidi Wapalestina 77 katika siku moja pekee
Jul 22, 2025 10:14Wizara ya Afya ya Palestina katika Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa: Katika muda wa saa 24 zilizopita, raia 77 wa Palestina wameuawa shahidi na wengine 376 kujeruhiwa katika mashambulizi ya utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
Papa ‘ashambuliwa’ kwa msimamo wake kuhusu kushambuliwa kanisa Ghaza
Jul 20, 2025 10:58Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Leo anaandamwa na ukosoaji mkali kutokana na mjibizo aliotoa kuhusiana na shambulio la anga lililofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel dhidi ya kanisa pekee la Kikatoliki katika Ukanda wa Ghaza.
-
Waziri wa zamani wa vita wa utawala wa Kizayuni akiri kutengwa Israel duniani
Jul 20, 2025 04:27Avigdor Lieberman waziri wa zamani wa vita wa utawala wa Kizayuni amekiri kuwa Israel na serikali inayoongozwa na Netanyahu zimetengwa kimataifa.
-
Marekebisho ya Taylor Greene ya kuacha kuusaidia utawala wa Kizayuni yapingwa katika Kongresi ya Marekani
Jul 20, 2025 00:07Baraza la Wawakilishi la Marekani limepinga marekebisho ya Marjorie Taylor Greene, mbunge katika baraza hilo, kwa ajili ya kupunguza msaada wa kijeshi wa dola milioni 500 kwa Israel.
-
Umoja wa Mataifa: Hali ya Gaza ni mbaya; kusitisha mapigano haitoshi
Jul 15, 2025 07:22Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ameitaja hali ya Gaza kuwa mbaya na kusema kuwa, usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza pekee hautoshi.
-
Kwa mara ya kwanza, Mahakama ya Uhispania yachunguza jinai za Netanyahu na wenzake
Jul 08, 2025 12:34Mahakama ya Taifa ya Uhispania imeanzisha uchunguzi wa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu anaoshutumiwa kuufanya waziri mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu, waziri wake wa vita Israel Katz, na maafisa kadhaa waandamizi wa jeshi la utawala huo haramu hususan shambulio la mwezi uliopita lililofanywa jeshi la kizayuni dhidi ya meli ya misaada ya kibinadamu.
-
Trump na Netanyahu wajadili kuwahamisha Wapalestina kwa nguvu Ghaza
Jul 08, 2025 12:29Waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu amekutana na Rais wa Marekani Donald Trump katika Ikulu ya White House, huku viongozi hao wawili wakirudia pendekezo lao tata la kuwahamisha kwa nguvu maelfu ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.
-
Israel yaharakisha kuifanya kaskazini ya Ghaza ibaki bila wakazi kabla vita kusimamishwa
Jul 06, 2025 16:04Duru za kuaminika za Palestina zimeripoti kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel unaharakisha kuhawamisha wakazi wa kaskazini ya Ghaza ili eneo hilo libaki tupu kabla ya kusimamishwa vita endapo mwafaka utafikiwa.