Apr 03, 2023 03:23
Kwa mnasaba wa Machi 30, Siku ya Ardhi ya Palestina, idadi kubwa ya raia wa Morocco walijumuika katika mji mkuu, Rabat na kushiriki katika maandamano ya kupinga utawala wa Kizayuni wa Israel, ambapo kwa mara nyingine wametaka kufutwa kwa mapatano ya kuanzishwa uhusiano wa kawaida kati ya serikali yao na utawala huo dhalimu.