-
Kila siku wanawake 600 hufanyiwa vitendo vya ukatili nchini Marekani
Nov 27, 2017 00:29Vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya wanawake katika nchi za Magharibi na hasa Marekani vimefikia kiwango cha kutia wasiwasi kinyume na inavyodaiwa huku ikiripotiwa kwamba kila siku wanawake 600 hufanyiwa vitendo vya ukatili nchini humo.
-
Iran: Wanawake ndio wahanga wakuu wa magenge ya kigaidi
Oct 28, 2017 04:36Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema wanawake ndio wahanga wakuu wa ukatili wa makundi ya kigaidi duniani.
-
Zaidi ya nusu ya wanawake Uingereza wanadhalilishwa kijinsia katika mazingira ya kazi
Oct 25, 2017 23:06Matokeo ya utafiti uliofanywa na televisheni ya BBC ya nchini Uingereza yanaonyesha kuwa, asilimia 53 ya wanawake nchini humo wanakumbwa na vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia wakiwa kazini na mashuleni hata hivyo waathirika wengi hawaripoti vitendo hivyo.
-
Baada ya marufuku ya miaka 60 hatimaye wanawake Saudia waruhusiwa kuendesha magari
Sep 27, 2017 01:19Baada ya malalamiko ya muda mrefu hatimaye Mfalme Salman bin Abdulaziz Al Saud wa Saudia ametoa amri ya kuwapa leseni za kuendesha magari wanawake wa nchi hiyo.
-
Watu 28 wauawa India, katika machafuko ya kupinga kuhukumiwa kiongozi wa Kihindu aliyebaka
Aug 25, 2017 23:29Polisi katika jimbo la Haryana nchini India imetangaza kuwa, kwa akali watu 28 wameuawa na wengine 200 kujeruhiwa vibaya katika mapigano yaliyotokea Ijumaa ya jana katika majimbo mawili ya Haryana na Punjab kaskazini mwa nchi hiyo.
-
UN yatiwa wasiwasi na hali za wanawake wa Kiiraqi katika miji inayokaliwa kwa mabavu na Daesh
Aug 22, 2017 23:17Ujumbe wa misaada ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa ulioko nchini Iraq na ofisi ya haki za binadamu ya umoja huo zimetoa ripoti na kutangaza kuwa wanawake na wasichana wa Kiiraqi wanaoishi kwenye miji inayokaliwa kwa mabavu na kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh wanakabiliwa na ukiukaji wa haki za binadamu.
-
FIBA yaruhusu mabinti wa Kiirani kushiriki katika mashindano ya kimataifa wakiwa na vazi la Hijabu
May 04, 2017 09:40Shirikisho la Mpira wa Kikapu Duniani (FIBA) limetangaza kuafiki pendekezo la Iran la kutaka wanawake wa Kiislamu na mabinti wenye Hijabu wa Kiirani kushiriki katika michezo ya kimataifa ya mpira wa kikapu (basketiboli).
-
HRW yapinga uanachama wa Saudia katika Baraza la Haki za Wanawake la UN
Apr 24, 2017 23:13Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) amepinga vikali uanachama wa utawala wa Saudi Arabia katika Baraza la Haki za Wanawake la Umoja wa Mataifa.
-
Wanawake wa Saudia waendeleza juhudi za kudai haki zao za msingi
Apr 06, 2017 03:00Wanawake wa Saudi Arabia wameendelea na juhudi za kudai haki zao za kijamii kukiwemo kuendesha magari binafsi, ambapo wameanzisha kampeni maalumu katika uwanja huo.
-
Kiongozi Muadhamu: Ni dharura kuelewa nafasi ya mwanamke wa Kiislamu katika jamii
Mar 19, 2017 13:02Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran, amesema kuna uwezekano mkubwa kwamba kumfanya mwanamke kuwa chombo cha anasa katika ulimwengu wa Magharibi, ni sehemu ya njama za Wazayuni kwa ajili ya kusambaratisha jamii ya mwanadamu.