-
Kikao kisichokuwa na natija cha Baraza la Usalama: Marekani yapinga usitishaji mapigano Gaza
Oct 19, 2023 10:50Jumatano, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilikataa tena azimio la kusitisha mapigano huko Gaza kufuatia upinzani wa Marekani. Marekani ilipinga azimio lililopendekezwa kwa Baraza la Usalama na Brazil, lililotaka kusitishwa mapigano ili kufikishwa misaada ya kibinadamu Ghaza.
-
Jitihada za Magharibi za kuzuia kuakisiwa habari za Wapalestina katika mitandao ya kijamii na vyombo vya habari
Oct 15, 2023 02:23Baada ya kuanza oparesheni kwa jina la "Kimbunga cha Al Aqsa" iliyotekelezwa na Hamas na makundi mengine ya mapambano ya Palestina; serikali na vyombo vya habari vya Magharibi kwa upande mmoja vimeanzisha propaganda kubwa ili kuzuia kuakisiwa habari na matukio yanayojiri huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu huku vikichapisha na kutoa habari za uwongo ili kuonyesha taswira isiyo ya kibinadamu kuhusu wanamapambano wa Palestina.
-
Msimamo tofauti wa Russia na China kuhusu operesheni ya Kimbunga cha al-Aqswa
Oct 12, 2023 02:31Licha ya uungaji mkono kamili wa Marekani na washirika wake wa magharibi kwa utawala wa Kizayuni wa Israel baada ya operesheni ya Kimbunga ya al-Aqswa na hata Washington kutuma misaada ya kijeshi na zana za kivita kwa utawala huo ghasibu, lakini Russia na China, yakiwa madola mawili hasimu na washindani wa Magharibi, yamechukua msimamo tofauti katika uwanja huu.
-
Taarifa rasmi ya Baraza la Usalama ya kulaani vitongoji vya walowezi
Feb 22, 2023 02:32Jumatatu ya tarehe 20 Februari Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipasisha rasimu ya azimio linalolaani uamuzi wa serikali ya Israel yenye misimamo ya kufurutu ada ya Benjamin Netanyahu wa kuidhinisha ujenzi wa vitongoji vipya tisa katika ardhi za Wapalestina za Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Kukataa utawala wa Kizayuni kushirikiana na Baraza la Haki za Binadamu la UN
Feb 20, 2022 02:52Utawala wa Kizayuni umekataa kushirikiana na Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa. Mwakilishi wa Israel katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ametangaza kuwa Tel Aviv haitashirikiana na jopokazi la uchunguzi la baraza hilo kwa ajili ya kuchunguza mashambulizi ya mwezi Mei mwaka jana ya utawala wa Kizayuni huko Ukanda wa Ghaza.
-
Amnesty International: Israel ni utawala wa ubaguzi wa rangi
Feb 02, 2022 11:30Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limeutuhumu utawala wa Kizayuni wa Israel kuwa ni utawala wa baguzi wa rangi wa apartheid. Amnesty Internation inakuwa taasisi ya karibuni zaidi ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu kuitangaza Israel kuwa ni utawala wa apartheid.
-
Ripoti ya Umoja wa Mataifa kuhusu jinai za Israel dhidi ya Wapalestina katika ardhi za mwaka 1948
Jun 05, 2021 02:28Katika ripoti yake mpya, Umoja wa Mataifa umefichua jinai mpya kadhaa zilizofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wanaoishi katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na Israel tangu mwaka 1948.
-
Ripoti ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa UN kuhusu jinai za Israel katika vita vya Gaza
May 29, 2021 03:02Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa Alkhamisi wiki hii alitoa ripoti yake kuhusu vita vya siku 12 vya Israel na mashambulizi ya kikatili ya utawala huo dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza huko Palestina.
-
Ufaransa yakiri kuhusu utambulisho wa kigaidi wa utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina
May 25, 2021 10:33Jumapili iliyopita Jean-Yves Le Drian, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa aliashiria hujuma ya kinyama iliyofanywa karibuni na utawala haramu wa Israel katika miji kadhaa ya Waarabu katika ardhi unazozikalia kwa mabavu na kutahadharisha dhidi ya ubaguzi wa rangi unaotekelezwa na utawala huo dhidi ya Wapalestina.
-
Silaha mpya za Marekani kwa utawala wa Israel; hatua nyingine ya kuendeleza mauaji dhidi ya Wapalestina
May 20, 2021 02:53Sambamba na kufikia kilele jinai za utawala wa kigaidi wa Israel dhidi ya Wapalestina, serikali ya Rais Joe Biden wa Marekani umeamua kuuzia utawala huo silaha mpya na za kisasa kabisa zenye thamani ya dola milioni 735.