Wanasiasa wa Pakistan: Ulimwengu wa Kiislamu unapaswa kusimama pamoja na Iran
https://parstoday.ir/sw/news/west_asia-i135458-wanasiasa_wa_pakistan_ulimwengu_wa_kiislamu_unapaswa_kusimama_pamoja_na_iran
Wanasiasa mbalimbali wa Pakistan wamesisitiza kuwa, ulimwengu wa Kiislamu unapaswa kuwa upande wa Iran katika mazingira ya sasa ambapo taifa hili la Kiislamu linaandamwa kwa njama mbalimbali.
(last modified 2026-02-15T09:07:51+00:00 )
Jan 14, 2026 02:41 UTC
  • Maulana Fazlur Rehman
    Maulana Fazlur Rehman

Wanasiasa mbalimbali wa Pakistan wamesisitiza kuwa, ulimwengu wa Kiislamu unapaswa kuwa upande wa Iran katika mazingira ya sasa ambapo taifa hili la Kiislamu linaandamwa kwa njama mbalimbali.

Akilaani vitisho vya Marekani na Israel dhidi ya Iran, mkuu wa chama cha Jamiat Ulema-e-Islami nchini Pakistan amesisitiza udharura wa ulimwengu wa Kiislamu kuiunga mkono Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

Maulana Fazlur Rehman, mkuu wa chama cha Jamiat Ulema-e-Islam nchini Pakistan, akijibu tabia ya vitisho ya Marekani na Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ametaka kuimarishwa kwa safu ya ulinzi ya pamoja na kusema: Ulimwengu wa Kiislamu lazima usimame na Iran katika wakati huu mgumu. Kulingana na Pars Today, Fazlur Rehman alisema katika taarifa yake mjini Lahore: Sasa ni wakati wa kuonyesha umoja imara wa Kiislamu na sote lazima tujibu vitisho hivi katika safu ya ulinzi ya pamoja. Aliongeza: Ulimwengu wa Kiislamu lazima ukusanyike chini ya mwavuli wa mkataba wa ulinzi wa pamoja.

Wakati huo huo, Sirajul Haq, kiongozi wa zamani wa Jamaat-e-Islami Pakistan, amelaani kauli za vitisho za Trump dhidi ya Iran na kusema: "Upuuzi wa Rais wa Marekani kuhusu kushambulia Iran unaonyesha njama ile ile ya zamani ya Wamarekani ya kupora akiba ya mafuta ya nchi nyingine huru."

Mushahid Hussain Syed, mchambuzi wa kisiasa na mwenyekiti wa zamani wa Kamati ya Ulinzi ya Seneti ya Pakistan, alisema katika mahojiano na Geo News huko Islamabad: "Marekani inapaswa kujua kwamba, Iran si Venezuela na kwamba juhudi za kuwachochea watu na kuushinikiza mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu zitashindwa." Alisisitiza: "Pakistan lazima isimame na umoja, uhuru, na umoja wa ardhi wa Iran, kupinga kuuondoa madarakani utawala halali au chaguo lolote la kijeshi na kukataa kuingiliwa na wageni."