-
Afrika Kusini: Mwanamume akiri kuwasha moto ulioua watu 76
Jan 25, 2024 04:02Mwanamume mmoja amekamatwa nchini Afrika Kusini na atakabiliwa na makosa 76 ya mauaji baada ya kuuambia uchunguzi kwamba alianzisha moto mbaya ulioteketeza jengo huko Johannesburg mwaka uliomalizika majuzi.
-
Afrika Kusini: Tunataraji ICJ itatoa hukumu ya kesi dhidi ya Israel Ijumaa
Jan 24, 2024 23:58Afrika Kusini imesema inatazamia hukumu ya kesi dhidi ya utawala haramu wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), kuhusu jinai za mauaji ya kimbari zinazotekelezwa na utawala huo dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza itatolewa Ijumaa ijayo.
-
Kuongezeka uungaji mkono wa kimataifa kwa mashtaka ya Afrika Kusini dhidi ya Israel
Jan 23, 2024 05:01Afrika Kusini ikiwa moja ya nchi wanachama wa Mkataba wa Kuzuia na Kuadhibu Uhalifu wa Mauaji ya Kimbari, iliwasilisha shauri la mashtaka dhidi ya Israel kwa Mahakama ya Kimataifa ya Haki mnamo Desemba 29, 2023.
-
Raisi: Iran inaunga mkono kesi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel ICJ
Jan 22, 2024 04:01Rais wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu inaunga mkono uamuzi wa 'busara' na wa 'kihistoria' wa Afrika Kusini wa kuwasilisha kesi dhidi ya utawala haramu wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ), kuhusu jinai za mauaji ya kimbari zinazotekelezwa na utawala huo dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Kesi iliyofunguliwa na A/Kusini dhidi ya Israel yaendelea kuungwa mkono
Jan 21, 2024 23:28Kwa mara nyingine tena, Ubelgiji imejiunga kwenye safu ndefu ya waungaji mkono wa hatua ya Afrika ya Kusini ya kufungua kesi dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ kutokana na jinai zake za kupindukia dhidi ya watoto wachanga, wanawake, vizee na watu wa kawaida huko Ghaza.
-
Kesi ya Afrika Kusini dhidi ya uhalifu wa Israel huko Gaza katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki
Jan 18, 2024 08:38Makaka yetu wiki hii itaangazia mashtaka yaliyowasilishwa na Afrika Kusini dhidi ya Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki, (IJC) kwa tuhuma za kufanya uhalifu wa kivita na mauaji ya kimbari dhidi ya watu wa Gaza huko Palestina.
-
Cuba yaunga mkono kesi iliyofunguliwa na Afrika Kusini dhidi ya utawala wa Kizayuni
Jan 18, 2024 06:01Bruno Rodríguez Parrilla Waziri wa Mambo ya Nje wa Cuba amesema kuwa Havana inaunga mkono mashtaka yaliyowasilishwa na Afrika Kusini katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kuhusu mauaji ya kimbari yaliyofanywa na utawala wa Israel dhidi ya watu wa Gaza.
-
Afrika Kusini kuzishtaki Marekani na Uingereza kwa kuhusika na jinai za kivita za Israel Gaza
Jan 16, 2024 03:35Baada ya Afrika Kusini kuwasilisha kesi dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) kwa kuhusika na mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza, mawakili wapatao 50 wa nchi hiyo wanatayarisha mashtaka mengine tofauti dhidi ya serikali za Marekani na Uingereza kwa msingi kwamba, serikali hizo zinahusika katika jinai na uhalifu unaofanywa na jeshi la Israel huko Gaza.
-
"Dunia ina wajibu wa kuunga mkono kesi ya Afrika Kusini dhidi ya Israel ICJ"
Jan 15, 2024 04:35Mwakilishi wa Slovenia katika Bunge la Ulaya amesema dunia ina jukumu la kuunga mkono kesi iliyowasilishwa na Afrika Kusini katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) dhidi ya Israel, kutokana na jinai na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Juhudi za utawala wa Kizayuni za kupotosha uhakika wa kutisha wa vita vya Gaza
Jan 13, 2024 08:46Kikao cha kusikiliza kesi iliyowasilishwa na Afrika Kusini dhidi ya Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki, ICJ, yenye makao yake huko Hague Uholanzi kimeanza katika hali ambayo mauaji ya kimbari na jinai za kivita za utawala wa Israel unaoiklia Quds kwa mabavu zingali zinaendelea katika ardhi za Palestina; na kila siku wananchi wa Palestina wanaendelea kuuliwa shahidi.