-
Vikosi vya Somalia vyaukomboa mji wa Runirgoud kutoka kwa magaidi wa Al-Shabaab
Dec 24, 2022 07:40Mashambulizi ya Jeshi la Somalia (SNA) dhidi ya kundi la magaidi wa Al-Shabaab yamepata mafanikio mapya baada ya vikosi vyake kuukomboa mji wa Runirgoud, ngome ya mwisho ya magaidi hao wakufurishaji huko Shabelle ya Kati, takriban kilomita 240 kaskazini mashariki mwa mji mkuu Mogadishu.
-
AU: Kundi la al-Shabaab linaelekea kusambaratika nchini Somalia
Nov 30, 2022 10:57Umoja wa Afrika umesema vitendo vya hivi karibuni vya kundi la kigaidi la al-Shabaab vya kuwalenga raia wasio na hatia katika mashambulizi yao vinaashiria namna genge hilo lilivyopoteza udhibiti wa ngome zake, kutokana na operesheni za Jeshi la Taifa la Somalia (SNA) na waitifaki wake.
-
Mzingiro wa al-Shabaab katika hoteli Somalia wahitimishwa, raia 9 na askari mmoja wauawa
Nov 29, 2022 07:53Vikosi vya usalama vya Somalia vimevamia hoteli moja katika mji mkuu Mogadishu ili kumaliza mzingiro wa siku moja wa wapiganaji wa al-Shabab ambao waliwaua watu tisa kwenye jengo lililoko karibu na makazi ya rais katika mji huo.
-
Wanamgambo 27 wa al Shabab wauawa katika shambulio la anga Somalia
Sep 23, 2022 07:52wanamgambo 27 kundi la kigaidi la al Shabab la nchini Somalia wameuawa katika shambulio la anga lililotekelezwa katika mkoa wa kati wa Hiran ambako jeshi la Somalia na majeshi waitifaki yalianzisha oparesheni dhidi ya kundi hilo mwezi uliopita.
-
Waliouawa katika shambulio dhidi ya hoteli Mogadishu wapindukia 20
Aug 22, 2022 04:24Watu wasiopungua 21 wameuawa huku wengine 117 wakijeruhiwa, baada ya kundi la kigaidi la la al-Shabaab kuwashika mateka mamia ya watu katika hoteli moja huko Mogadishu, mji mkuu wa Somalia.
-
Al-Shabaab yaua watu 17 katika shambulio karibu na Ethiopia
Jul 22, 2022 03:12Kundi la kigaidi la al-Shabaab la Somalia limefanya shambulio nadra karibu na nchi jirani ya Ethiopia, lililopelekea kuuawa watu wasiopungua 17, wakiwemo raia watatu.
-
Rais wa Somalia: Ukifika wakati mwafaka tutafanya mazungumzo na Ash-Shabaab
Jul 08, 2022 02:08Rais mpya wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud amesema, kuhitimisha uasi wa utumiaji silaha unaofanywa na kundi la Ash-Shabaab unahitaji mbinu nyingine kuliko ya kijeshi na kwa hivyo utakapofika wakati mwafaka, serikali yake itafanya mazungumzo na kundi hilo lenye misimamo ya kufurutu ada.
-
Shambulio la kundi la kigaidi la as-Shabaab dhidi ya askari wa kulinda amani nchini Somalia
May 05, 2022 05:30Jeshi la Burundi limetangaza kuwa askari wake 10 wa kulinda amani wanaohudumu nchini Somalia chini ya mwavuli wa Umoja wa Afrika wameuawa katika shambulio lililotekelezwa na kundi la kigaidi la as-Shabaab katika kambi ya askari wa umoja huo.
-
Watu 3 wauliwa katika shambulio la al Shabab katika kambi ya AU Somalia
May 04, 2022 08:12Kundi la wanamgambo wa al Shabab lenye makao yake nchini Somalia limeishambulia kambi ya wanajeshi wa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika (AU) katika mkoa wa Shabelle katikati ya Somalia.
-
Magaidi 7 wa al-Shabaab waangamizwa na jeshi la Somalia eneo la Mudug
Apr 04, 2022 11:23Kikosi maalumu cha Danab cha Jeshi la Taifa la Somalia (SNA) kimefanikiwa kuwaangamiza wanachama saba wa kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab katikati ya nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.