-
Answarullah: Jinai za Saudia nchini Yemen zimeifedhehesha UN na asasi za kimataifa
Aug 24, 2018 08:14Mkuu wa Kamati Kuu ya Mapinduzi ya Yemen amelaani vikali shambulizi la kinyama la ndege za muungano vamizi wa Saudi Arabia katika mkoa wa Al-Hudaydah na kusema kuwa hujuma hizo zimezifedhehesha mno asasi za kimataifa pamoja na Umoja wa Mataifa kutokana na udhaifu wake.
-
Answarullah: Magaidi ni jeshi la pili la Saudi Arabia
Aug 18, 2018 04:25Muhammad Ali al Houthi, Mkuu wa Kamati Kuu ya Mapinduzi ya Yemen amelaani taarifa ya kutangazwa uungaji mkono wa kifedha wa Saudia kwa muungano wa kimataifa wa kijeshi wa eti kupambana na Daesh unaoongozwa na Marekani nchini Syria na kusema, magaidi ni jeshi la pili la Riyadh.
-
Ansarullah yalaani kufukuzwa balozi wa Canada nchini Saudia, yamkaribisha Yemen
Aug 06, 2018 08:06Mkuu wa Kamati Kuu ya Mapinduzi ya Yemen amelaani kitendo cha Saudi Arabia cha kumfukuza balozi wa Canada mjini Riyadh na kuitaka Ottawa kufungua ubalozi wake San'a, mji mkuu wa Yemen.
-
Ansarullah: Tutaigeuza miji ya pwani ya magharibi mwa Yemen kuwa makaburi ya wavamizi
Aug 05, 2018 08:08Msemaji wa harakati ya Ansarullah ya Yemen ametangaza kuwa, harakati hiyo itaigeuza miji ya pwani ya magharibi mwa nchi hiyo kuwa makaburi ya vikosi vamizi vinavyoongozwa na Saudi Arabia.
-
Msemaji wa Ansarullah ya Yemen: UAE ni kibaraka wa Marekani
Jul 30, 2018 14:24Msemaji wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amesema: Bila Marekani, Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) si lolote si chochote na ni dhaifu mno kuweza hata kupigana vita na kijiji kimoja cha Yemen.
-
Utayarifu wa Yemen kwa ajili ya kushadidisha mashambulizi dhidi ya wavamizi
Jul 07, 2018 11:01Mohammed Abdulsalam msemaji rasmi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amebainisha kwamba vikosi vya kujitolea vya wananchi na jeshi la nchi hiyo vipo tayari kushadidisha mashambulizi dhidi ya muungano vamizi unaoongozwa na Marekani na Saudi Arabia katika maeneo mbalimbali ya Yemen.
-
Ansarullah: Madai ya Imarati ya kusimamisha hujuma zake Hudaydah ni urongo
Jul 02, 2018 07:00Harakati ya Ansarullah ya Yemen imekadhibisha madai yaliyotolewa na Umoja wa Falme za Kiarabu kwamba eti imesitisha oparesheni ya kutaka kukalia kwa mabavu mji wa bandari wa al-Hudaydah nchini Yemen.
-
Answarullah: Sio kweli kwamba tumekubali kuukabidhi Umoja wa Mataifa bandari ya Al Hudaydah
Jun 28, 2018 13:41Harakati ya Wananchi ya Answarullah nchini Yemen imekadhibisha baadhi ya habari za vyombo vya habari vya nchi za Magharibi kwamba imekubali kukabidhi usimamizi wa bandari ya Al Hudaydah kwa Umoja wa Mataifa.
-
Tathmini ya Abdul Malik al Houthi kuhusu vita dhidi ya bandari ya al Hudaydah nchini Yemen.
Jun 16, 2018 06:53Abdul Malik al Houthi, Katibu Mkuu wa Harakati ya Answarullah ya Yemen ametoa hotuba maalumu kwa mnasaba wa sikukuu ya Idul Fitr na kutathmmini matukio ya hivi karibuni ya Yemen na medani ya vita katika mji wa bandari wa al Hudaydah akisisitiza kuwa Israel, Marekani na Saudi Arabia zote zinashiriki kikamilifu katika vita hivyo.
-
Ansarullah: Al-Hudaydah itakuwa makaburi ya askari vamizi
Jun 15, 2018 04:37Kiongozi wa ngazi ya juu wa Harakati ya wananchi ya Ansarullah nchini Yemen amesema kuwa, shambulizi dhidi ya meli ya kivita ya Saudi Arabia katika pwani ya al-Hudaydah ni jibu imara dhidi ya wavamizi linalotoa ujumbe wa wazi kwamba, eneo hilo litakuwa makaburi ya askari vamizi.