Jan 06, 2024 10:52
Maadhimisho ya miaka mitatu ya shambulio dhidi ya Bunge la Congress ya Marekani Januari 6, 2021 yamewadia huku wapinzani wawili katika uchaguzi wa rais, ambao ni Rais Mdemocrati, Joe Biden, na mgombea mkuu wa chama cha Republican, Donald Trump, wakishambuliana kwa maneno makali hasa katika kipindi hiki cha kuingia mwaka wa uchaguzi wa rais nchini Marekani.