-
Mapigano baina ya wapinzani na waungaji mkono wa Trump mjini Washington
Nov 15, 2020 07:55Maandamano ya wafuasi na waungaji mkono wa Rais Donald Trump wa Marekani wanaopinga matokeo ya uchaguzi wa rais uliofanyika tarehe 3 mwezi huu wa Novemba yameufanya mji wa Washington kuwa uwanja wa mapaigano baina ya wafuasi na wapinzani wa kiongozi huyo.
-
Ghalibaf: Kasi ya kuporomoka Marekani imeongezeka
Nov 15, 2020 04:42Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa, matukio yaliyoambatana na uchaguzi wa Marekani yamezidi kuporomosha itibari ya nchi hiyo na kuongeza kasi ya kuporomoka mfumo wa kibeberu wa Marekani.
-
Trump kushiriki maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi Marekani
Nov 14, 2020 03:51Rais anayeondoka wa Marekani, Donald Trump amesema yumkini leo atajiunga na wafuasi wake katika maandamano ya mjini Washington, ya kupinga mchakato na matokeo ya uchaguzi wa rais uliofanyika mwezi uliopita.
-
Wito wa kuhitimishwa sarakasi za uchaguzi wa rais wa Marekani
Nov 14, 2020 03:16Kuendelea kwa mzozo wa matokeo ya uchaguzi wa rais wa Marekani uliozushwa na Rais Donalld Trump ambaye alikuwa mgombea wa chama cha Republican katika uchaguzi huo, kupanuka mzozo huo na kutolewa madai mapya kumetajwa kuwa ni tahadhari kubwa kuhusiana na matokeo mabaya kwa Marakeni.
-
Marekani yakerwa na kuchunguzwa rekodi yake mbovu ya haki za binadamu katika Umoja wa Mataifa
Nov 13, 2020 05:38Marekani ambayo ni mmoja wa wakiukaji wakubwa zaidi wa haki za binadamu duniani, ina historia nyesu kuhusu jambo hilo na daima imekuwa ikiingilia masuala ya ndani na kuzikosoa nchi nyingine ili kujaribu kukwepa kuwajibika mbele ya Wamarekani na walimwengu kwa ujumla kuhusu suala hilo.
-
Vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Iran, muendelezo wa njama za aliyeshindwa
Nov 12, 2020 07:13Baada ya Donald Trump kuitoa Marekani katika mapatano ya kimataifa ya nyuklia yajulikanayo kwa jina la JCPOA hapo mwezi Mei 2018, Washington iliiwekea Iran vikwazo vya kiwango cha juu na hadi leo hii, kila siku inaweka vikwazo vipya.
-
Nasrullah: Utawala wa Trump ndio mbaya zaidi katika historia ya Marekani
Nov 12, 2020 03:57Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema utawala wa rais anayeondoka wa Marekani, Donald Trump ndiyo serikali mbaya zaidi katika historia ya nchi hiyo.
-
Iran: Hatuogopi Trump akibaki wala hatutasisimuka Biden akiingia madarakani
Nov 11, 2020 04:23Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameashiria matukio ya sasa ya uchaguzi wa rais nchini Marekani na kusema: "Hatuogopi iwapo Trump atabakia na wala hatutasisimuka iwapo Biden ataingia madarakani. Tunachukua maamuzi kwa mujibu wa maslahi yetu."
-
Kuuzuliwa Waziri wa Ulinzi wa Marekani; pigo jingine kwa serikali inayotetereka ya Trump
Nov 10, 2020 23:07Rais Donald Trump wa Marekani ambaye alishika hatamu za uongozi wa nchi hiyo akitokea nje ya mzunguko wa kisiasa, katika uga wa timu yake ya uongozi pia amekuwa na utendaji wa ajabu na ambao haujazoeleka.
-
Trump amfuta kazi Waziri wa Ulinzi, wasomi waonya dhidi ya hatua za rais huyo wa US
Nov 10, 2020 04:40Katika hali ambayo mgogoro unaendelea kutotoka nchini Marekani baada ya Joe Biden kutangazwa mshindi wa uchaguzi wa rais huku Donald Trump akipinga matokeo hayo kwa madai kuwa uchaguzi uligubikwa na wizi wa kura, rais huyo anayeondoka wa US amempiga kalamu nyekundu Waziri wa Ulinzi, Mark Esper.