-
Hamas: Kuongezeka mashambulizi dhidi ya Gaza ni jaribio la kuua makubaliano ya kusitisha mapigano
Jul 24, 2026 07:13Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imetangaza kwamba mashambulizi makubwa ya anga ya utawala wa Israel eneo la Ukanda wa Gaza katika saa kadhaa zilizopita ni mwendelezo wa vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya raia wasio na hatia na msisitizo wa kuvuruga makubaliano ya kusitisha mapigano.
-
Israel yafanya mauaji makubwa huko Nuseirat, janga la binadamu linazidi kuwa baya Gaza
Jul 18, 2026 10:59Wapalestina 14 wameuawa na wengine 37 kujeruhiwa, wengi wao wakiwa katika kambi ya Nuseirat katikati mwa Ukanda wa Gaza, kutokana na mashambulizi mtawalia ya Israel yaliyolenga maeneo mbalimbali ya ukanda huo, huku hali ya kibinadamu ikizidi kuwa mbaya.
-
Madaktari na wauguzi wa London wataka kuachiliwa huru daktari wa watoto wa Kipalestina
Jul 13, 2026 03:08Madaktari, wauguzi na wanaharakati wamekusanyika nje ya Chuo cha Kifalme cha Watoto na Afya ya Watoto (RCPCH) jijini London, wakitaka hatua zichukuliwe dhidi ya kukamatwa kinyume cha sheria daktari wa watoto wa Kipalestina Dkt. Hussam Abu Safiya anayeshilikiwa na utawala ghasibu wa Israel.
-
Seneta Graham, msaidizi mkuu wa Trump na mchochezi mkuu wa vita dhidi ya Iran ameangamia ghafla
Jul 12, 2026 10:17Seneta Lindsey Graham, anayetambuliwa kuwa mhandisi wa mipango ya Washington dhidi ya Iran na mhamasishaji mkuu wa Trump kufanya mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu, hatimaye ameangamia na ndoto yake ya kunyakua "matrilioni ya dola katika pesa na mafuta ya Iran."
-
Trump amwambia Netanyahu katika malumbano makali ya simu: "Wayahudi wote wamekuchoka"
Jun 26, 2026 11:16Televisheni ya CNN ya Marekani imefichua malumbano makali ya simu baina ya Rais wa Marekani na Waziri Mkuu wa Israel ambapo Donald Trump amemkemea Benjamin Netanyahu, akimwambia: "Wayahudi wote wamekuchoka," huku Marekani ikizidisha mashinikizo kwa ajili ya kufikia makubaliano kuhusu Ukanda wa Gaza.
-
Jihad Islami yailaumu Marekani kwa ukatili unaoendelezwa na Israel huko Gaza
Jun 19, 2026 03:50Harakati ya Jihadi Islami ya Palestina imesema utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani lazima uwajibishwe kwa ukatili na vitendo vya uchokozi vinavyofanywa na askari wa utawala vamizi wa Israel dhidi ya Wapalestina wa kawaida katika Ukanda wa Gaza ulioharibiwa na vita.
-
Wapiga picha wa Gaza washinda Tuzo ya Kalamu ya Dhahabu ya Uhuru
Jun 15, 2026 11:19Jumuiya ya Wachapishaji Habari Duniani imetangaza kwamba tuzo ya Kalamu ya Dhahabu ya Uhuru 2026 itatolewa kwa wapiga picha na wakurugenzi wa video kutoka Ukanda wa Gaza ulioharibiwa na vita.
-
Italia yaanzisha uchunguzi dhidi ya Ben-Gvir kuhusu unyanyasaji wa wanaharakati wa Global Sumud Flotilla
Jun 10, 2026 03:59Waendesha mashtaka wa Italia wameanzisha uchunguzi dhidi ya Waziri wa Usalama wa Israel mwenye msimamo mkali wa mrengo wa kulia, Itamar Ben-Gvir kuhusu mateso, unyanyasaji na utekaji nyara wa wanaharakati walioshiriki katika msafara wa Global Sumud Flotilla wa kupeleka misaada ya kibinadamu kwa watu wa Gaza, mwezi uliopita.
-
Guterres: Wafanyakazi 80 wa Umoja wa Mataifa waliuawa mwaka jana huko Gaza
Jun 09, 2026 11:46Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, ametangaza kwamba wafanyakazi 136 wa shirika hilo la kimataifa waliuawa wakitekeleza majukumu yao katika mwaka uliopita, wakiwemo wafanyakazi 80 waliokuwa wakifanya kazi katika Ukanda wa Gaza huko Palestina.
-
Waandishi wa habari wa Gaza wasimulia unyanyasaji waliokumbana nao katika gereza la Israel
Jun 07, 2026 03:50Shirika la Waandishi wa Habari Wasio na Mipaka (RSF) limechapisha ushuhuda kutoka kwa waandishi wa habari watano wa Kipalestina huko Gaza, ambao walitekwa nyara na askari wa Israel baada ya Oktoba 7, 2023 ikiwa ni pamoja na visa vya unyanyasaji, kuhojiwa na ukiukwaji wa sheria unaohusiana moja kwa moja na shughuli zao za uandishi wa habari.