-
Jamii ya Wangazija yapiganiwa itambuliwe rasmi nchini Kenya
Aug 08, 2025 08:09Seneta wa Kaunti ya Mombasa iliyoko eneo la pwani ya Kenya ametoa wito wa kutaka suala la jamii ya Wangazija kutatuliwa na kupewa haki kama watu wengine nchini humo.
-
HAMAS yamsuta Witkoff, yasema haitaweka chini silaha mpaka iundwe nchi huru ya Palestina
Aug 03, 2025 02:12Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imekanusha madai yaliyotolewa na mjumbe wa Marekani Mashariki ya Kati Steve Witkoff kwamba ilionyesha nia ya kuwa tayari kukabidhi silaha zake wakati wa mazungumzo ya kusitisha mapigano Ghaza kati yake na Israel, ikisisitiza kwamba ina haki ya "kitaifa na kisheria" kukabiliana na uvamizi wa utawala huo wa kizayuni katika ardhi ya Palestina.
-
Wapalestina 1373 wauawa shahidi wakisubiri msaada wa chakula Gaza
Aug 02, 2025 23:07Ofisi ya Kamisheni Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa imetangaza kuwa: Tokea tarehe 27 Mei mwaka huu hadi sasa Wapalestina 1373 wameuliwa shahidi katika Ukanda wa Gaza wakati walipokuwa wakisubiri kugawiwa msaada wa chakula. Waliuliwa shahidi kwa kufyatiliwa risasi na wanajeshi wa Kizayuni.
-
Uholanzi yawazuia kuingia nchini Ben-Gvir na Smotrich kwa kuchochea machafuko na maangamizi ya kizazi Ghaza
Jul 29, 2025 23:24Uholanzi imewataja mawaziri wa Israeli Itamar Ben-Gvir na Bezalel Smotrich kuwa watu wasiokubalika na hivyo imewapiga marufuku kuingia nchini humo kutokana na vitendo vyao vya kuwachochea walowezi wa Kizayuni kuendesha ghasia na vitendo vya mabavu dhidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi na maangamizi ya kizazi katika Ukanda wa Gaza.
-
Wapalestina waliouliwa shahidi na jeshi la kizayuni Ghaza wakaribia 60,000; 92 wauawa kwa siku moja
Jul 29, 2025 03:31Idadi ya Wapalestina waliouwa shahidi kwa mashambulizi ya kinyama ya jeshi la utawala wa kizayuni katika Ukanda wa Ghaza inakaribia 60,000 baada ya jeshi hilo katili kuwaua Wapalestina wengine 92 katika muda wa siku moja wakiwemo 41 waliokuwa wakihangaika kupata msaada wa chakula.
-
Wananchi wa Morocco, Tunisia na Iraq waandamana kuwaunga mkono watu wa Gaza
Jul 27, 2025 23:12Wananchi wa Morocco, Tunisia na Iraq wawameandamana katika miji mikuu ya nchi hizo kuonyesha mshikamano na wananchi wa Gaza wakisisitiza kuondolewa mzingiro wa eneo hilo na kukomeshwa sera za utawala wa Kizayuni za kuwasababishia njaa wakazi madhulumu wa eneo hilo.
-
Wapalestina 127 wameshakufa shahidi kutokana na njaa na lisheduni katika Ukanda wa Ghaza
Jul 27, 2025 07:38Maafisa wa utoaji misaada katika Ukanda wa Ghaza wametangaza leo kuwa watu 127 wamekufa shahidi kwa utapiamlo na njaa kutokana na mzingiro mkubwa lililowekewa eneo hilo na utawala wa kizayuni na hatua ya utawala huo ghasibu ya kuzuia uingizaji misaada ya kibinadamu.
-
Mabomu ni ghali, risasi ni bei nafuu! Mkakati wa Marekani na Israel wa kuwaua Wapalestina katika safu za chakula
Jul 16, 2025 13:20Katika mwezi wa 23 wa Vita vya Gaza, ambapo utawala wa Kizayuni wa Israel umefanya mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza kwa ukatili na unyama wa hali ya juu na kwa kutumia silaha ya njaa, sasa utawala huo umebuni mbinu mpya kwa ajili ya kile kinachojulikana kama 'mauaji ya bei nafuu' ya wakazi wa Gaza.
-
Waliouawa shahidi Ghaza wapindukia 58,000, Israel yaendeleza mashambulizi ya kinyama bila ya khofu
Jul 14, 2025 00:38Wapalestina wasiopungua 58,026 wameshuawa shahidi katika vita vya kinyama na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa kizayuni wa Israel kwenye Ukanda wa Gaza tangu Oktoba 2023.
-
Sababu za Marekani na Israel kuwapiga risasi Wapalestina kwenye safu za misaada huko Gaza
Jul 05, 2025 22:55Wakandarasi wa usalama wa Marekani wanatumia risasi za moto, maguruneti, na gesi ya kuwasha dhidi ya raia katika vituo vya usambazaji wa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza.