-
Kukaririwa mauaji ya utawala wa Kizayuni dhidi ya watoto huko Marekani kwa kuuawa kinyama mtoto wa Kipalestina
Oct 16, 2023 08:43Polisi ya Chicago imetangaza kuwa mkazi mmoja wa mji huo amemuua mvulana wa Kipalestina wa miaka 6 kwa kisu na kumjeruhi vibaya mama yake.
-
Jitihada za Magharibi za kuzuia kuakisiwa habari za Wapalestina katika mitandao ya kijamii na vyombo vya habari
Oct 14, 2023 22:53Baada ya kuanza oparesheni kwa jina la "Kimbunga cha Al Aqsa" iliyotekelezwa na Hamas na makundi mengine ya mapambano ya Palestina; serikali na vyombo vya habari vya Magharibi kwa upande mmoja vimeanzisha propaganda kubwa ili kuzuia kuakisiwa habari na matukio yanayojiri huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu huku vikichapisha na kutoa habari za uwongo ili kuonyesha taswira isiyo ya kibinadamu kuhusu wanamapambano wa Palestina.
-
Tovuti ya Marekani "The Grayzone" yafichua chanzo cha uongo wa Biden kuhusu kukatwa vichwa watoto wa Israel
Oct 12, 2023 08:38Tuvuti ya habari ya Marekani imefichua ukweli kuhusu uongo uliosemwa na Rais Joe Biden alipodai kuwa wanachama wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) waliwakata vichwa watoto wadogo wakati wa operesheni ya kijeshi ya Kimbunga cha al Aqsa Jumamosi iliyopita.
-
Hamas yajibu matamshi ya kichochezi ya Biden juu ya Palestina
Oct 11, 2023 23:02Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imekosoa vikali matamshi yaliyotolewa na Rais Joe Biden wa Marekani na kusisitiza kuwa, matamshi hayo ya kichochezi yanalenga kukoleza moto wa jinai za utawala katili wa Israel dhidi ya Wapalestina.
-
Jeshi la Israel lakiri: Zaidi ya Wazayuni 1,200 wameuawa
Oct 10, 2023 23:29Jeshi la utawala haramu wa Israel limeungama na kusema kuwa Wazayuni zaidi ya elfu moja na 200 wameangamizwa na wapiganaji wa makundi ya mapambano ya Palestina, tangu Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa ilipoanza Jumamosi iliyopita.
-
Hatua za kichochezi za Marekani kuunga mkono utawala wa Kizayuni
Oct 09, 2023 06:16Kufuatia mashambulizi makubwa ya makundi ya mapambano na ukumbozi wa Palestina katika maeneo yanayouzunguka Ukanda wa Ghaza, ambayo yamedhihirisha udhaifu na utepetevu mkubwa wa utawala wa Kizayuni, Marekani imepanga na kutekeleza hatua za kichochezi kwa kisingizio cha eti kuiunga mkono Tel Aviv na kuimarisha ari ya Wazayuni.
-
Undani wa oparesheni ya Kimbunga cha Al Aqsa kwa upande wa kijeshi na kiitelijinsia
Oct 09, 2023 04:43Makundi ya muqawama ya Palestina yenye makao katika Ukanda wa Ghaza yaani harakati ya Hamas na harakati nyingine za Palestina khususan Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina juzi Jumamosi tarehe 7 Oktoba yalianzisha oparesheni kwa jina la Kimbunga cha Al Aqsa dhidi ya utawala wa Kizayuni; oparesheni iliyouduwaza kikamilifu utawala huo na kuwashtua pakubwa Wazayuni.
-
Haniya: Kimbunga cha Al-Aqsa kimeanzia Gaza na kitafika hadi Ufukwe wa Magharibi
Oct 07, 2023 11:44Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema: Kimbunga cha Al-Aqsa kimeanzia Gaza na kitafika hadi Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, nje yake na popote pale walipo wananchi wa Palestina.
-
HAMAS yataka kuendelezwa muqawama dhidi ya Wazayuni
Sep 30, 2023 01:07Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imesema kuna haja ya kuendeleza muqawama na mapambano dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
HAMAS yalaani kauli ya Katibu Mkuu wa UN kuyaita mapambano ya Wapalestina 'vurugu na utumiaji nguvu'
Sep 15, 2023 09:56Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imekosoa vikali kauli ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ya kuuita Muqawama wa wananchi wa Palestina dhidi ya utawala ghasibu wa Israel kuwa ni "vurugu" na kusisitiza kwamba kinachofanyika katika ardhi za Palestina ni haki ya kujihami dhidi ya utawala unaokalia ardhi kwa mabavu.