-
Hatua za kichochezi za Marekani kuunga mkono utawala wa Kizayuni
Oct 09, 2023 06:16Kufuatia mashambulizi makubwa ya makundi ya mapambano na ukumbozi wa Palestina katika maeneo yanayouzunguka Ukanda wa Ghaza, ambayo yamedhihirisha udhaifu na utepetevu mkubwa wa utawala wa Kizayuni, Marekani imepanga na kutekeleza hatua za kichochezi kwa kisingizio cha eti kuiunga mkono Tel Aviv na kuimarisha ari ya Wazayuni.
-
Undani wa oparesheni ya Kimbunga cha Al Aqsa kwa upande wa kijeshi na kiitelijinsia
Oct 09, 2023 04:43Makundi ya muqawama ya Palestina yenye makao katika Ukanda wa Ghaza yaani harakati ya Hamas na harakati nyingine za Palestina khususan Harakati ya Jihadul Islami ya Palestina juzi Jumamosi tarehe 7 Oktoba yalianzisha oparesheni kwa jina la Kimbunga cha Al Aqsa dhidi ya utawala wa Kizayuni; oparesheni iliyouduwaza kikamilifu utawala huo na kuwashtua pakubwa Wazayuni.
-
Haniya: Kimbunga cha Al-Aqsa kimeanzia Gaza na kitafika hadi Ufukwe wa Magharibi
Oct 07, 2023 11:44Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema: Kimbunga cha Al-Aqsa kimeanzia Gaza na kitafika hadi Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, nje yake na popote pale walipo wananchi wa Palestina.
-
HAMAS yataka kuendelezwa muqawama dhidi ya Wazayuni
Sep 30, 2023 01:07Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imesema kuna haja ya kuendeleza muqawama na mapambano dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
HAMAS yalaani kauli ya Katibu Mkuu wa UN kuyaita mapambano ya Wapalestina 'vurugu na utumiaji nguvu'
Sep 15, 2023 09:56Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imekosoa vikali kauli ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ya kuuita Muqawama wa wananchi wa Palestina dhidi ya utawala ghasibu wa Israel kuwa ni "vurugu" na kusisitiza kwamba kinachofanyika katika ardhi za Palestina ni haki ya kujihami dhidi ya utawala unaokalia ardhi kwa mabavu.
-
Muqawama: Hatutafumbia macho upuuzi wa kuwadhalilisha wanawake Wapalestina
Sep 08, 2023 03:58Makundi ya muqawama ya Palestina yameapa kulipiza kisasi cha kudhalilishwa wanawawake wa Kipalestina katika mji wa al-Khalil, eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan linalokaliwa kwa mabavu.
-
Haniya: Israel inabeba dhima ya mauaji katika jamii ya Waarabu
Sep 03, 2023 03:53Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema utawala haramu wa Israel unabeba dhima ya mauaji ya kiholela katika jamii ya Waarabu katika ardhi za Wapalestina zinazokaliwa kwa mabavu.
-
HAMAS: Operesheni za silaha dhidi ya Israel hazitasimama
Aug 20, 2023 03:08Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imesisitiza kuwa, kambi ya muqawama itaendelea kufanya operesheni zao za kimapambano kwa kutumia silaha dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Hamas: Kadhia ya Palestina inakabiliwa na changamoto ya aina yake
Aug 10, 2023 03:35Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imeeleza kuwa suala la Palestina linakabiliwa na changamoto ambayo haijawahi kushuhudiwa.
-
Hamasa: Kuripua nyumba za raia wa Palestina ni ishara ya udhaifu wa Wazayuni
Aug 08, 2023 23:43Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imelaani jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel za kuripua nyumba za mashahidi wa Palestina na kusisitiza kuwa, sera hizo za viongozi wa Tel Aviv ni ishara ya kutojiweza utawala wa Kizayuni.