-
HAMAS yasisitiza kuimarisha uhusiano wake na Iran na Hizbullah ya Lebanon
Jan 21, 2018 10:40Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amesema uhusiano wa harakati hiyo na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na harakati ya Hizbullah ya Lebanon umerejea kwenye mkondo wake wa kawaida.
-
Haniya amuandikia barua Kiongozi Muadhamu akipongeza msimamo wa Iran kuhusu Quds
Jan 18, 2018 10:56Kiongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amemuandikia barua Kiongozi Mudhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu akishukuru na kupongeza msimamo wa Iran kuhusu Quds Tukufu.
-
Hamas yaitaka PLO kuutekeleza kivitendo uamuzi wake
Jan 17, 2018 01:00Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imetangaza kuwa, uamuzi wa Harakati ya Ukombozi wa Palestina PLO kuhusiana na tangazo la Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu Beitul-Muqaddas utakkuwa na umuhimu pale PLO itakapoutekeleza kivitendo.
-
Hamas: Huenda Trump akaitambua Israel kama dola la Kiyahudi
Dec 24, 2017 04:34Kiongozi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas, Ismail Haniya amesema amepokea taarifa za siri kuwa Washington inapanga kuutambua utawala haramu wa Israel kama dola la Kiyahudi.
-
Hamas yakaribisha takwa la ANC la kupunguzwa uhusiano wa kidiplomasia wa Afrika Kusini na Israel
Dec 22, 2017 12:13Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imekaribisha kwa mikono miwili takwa la chama tawala nchini Afrika Kusini ANC kwa serikali ya nchi hiyo la kupunguzwa kiwango cha ushirikiano wa kidiplomasia wa nchi hiyo na utawala ghasibu wa Israel.
-
Hamas: Kushambuliwa Ghaza; ni njama zilizofeli za kutaka kuzima Intifadha ya Quds
Dec 18, 2017 23:19Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas imetangaza kuwa mashambulizi makubwa ya ndege za kivita za utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghaza ni njama zilizofeli za kutaka kuzima mapambano ya Intifadha ya kuiunga mkono Quds katika ardhi zote za Palestina.
-
Harakati ya Hamas yaionya Israel kuhusiana na jinai zake dhidi ya Wapalestina
Dec 16, 2017 00:38Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa radiamali yake kuhusiana na jinai ya utawala dhalimu wa Israel ya kuwaua shahidi Wapalestina kadhaa katika maandamanao ya jana ya 'Ijumaa ya Ghadhabu' na kuuonya utawala huo kuhusiana na jinai zake dhidi ya Wapalestina.
-
Hamas: Hakuna nchi inayoitwa 'Israel' hata mji mkuu wake uwe 'Quds'
Dec 14, 2017 12:31Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imelaani vikali uamuzi wa Rais wa Marekani, Donald Trump wa kuitangaza Baytul Muqaddas kuwa mji mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel na kusisitiza kuwa, hakuna dola linaloitwa Israel hata mji mkuu wake uwe Quds tukufu.
-
Hamas yasema kesho ni 'Ijumaa ya Ghadhabu' ya kuihami Quds
Dec 07, 2017 11:20Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina Hamas imeutaja uamuzi wa Rais wa Marekani, Donald Trump wa kuitangaza Baytul Muqaddas kuwa mji mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel kama tangazo la vita huku ikisema kuwa kesho itakuwa Ijumaa ya Ghadhabu na fursa kwa ulimwengu wa Kiislamu kuonyesha hasira zao dhidi ya Washington na Tel Aviv.
-
Hamas yakosoa hatua ya Israel ya kuzuia ujumbe wa Uswisi kutembelea Ukanda wa Ghaza
Nov 30, 2017 12:48Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kuwa kitendo cha utawala wa Kizayuni wa Israel cha kuzuia ujumbe wa Uswisi kulitembelea eneo la Ukanda wa Ghaza kwa ajili ya kuonana na wawakilishi na wananchi wa eneo hilo si cha kibinadamu na kinakiuka haki za wananchi wa Palestina.