-
Hizbullah yaapa kujibu mashambulizi ya Israel yaliyoua raia wakiwemo watoto wawili
Feb 15, 2024 04:19Afisa wa ngazi ya juu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amelaani mashambulizi ya hivi karibuni zaidi ya Israel kusini mwa Lebanon yaliyosababisha vifo vya watu kadhaa wakiwemo watoto wawili, ikiapa kwamba majibu ya harakati ya Muqawama ya Lebanon yako njiani.
-
Hizbullah yaonya dhidi ya sera ya kupenda vita ya Israel
Feb 12, 2024 01:07Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema mrengo wa muqawama haujatangaza vita kamili, lakini iwapo Israel itapanua vita vyake vya Gaza, wanamuqawama hawatasita kufanya mashambulizi ya kujibu chokochoko za adui huyo mpenda vita.
-
Hizbullah: Njia pekee ya kuondoa wasiwasi ni kukomeshwa mauaji ya kimbari Ghaza
Feb 02, 2024 23:38Naibu Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, harakati hiyo imejiweka tayari kukabiliana na vitisho vyovyote vya utawala wa Kizayuni na kusisitiza kuwa, njia pekee ya kuondoa wasiwasi uliopo ni Israel kukomesha mauaji ya watu wasio na hatia huko Ghaza, Palestina.
-
Makombora ya Hizbullah ya Lebanon yapiga ngome za kijeshi za Israel
Jan 27, 2024 08:33Wapiganaji wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon wameshambulia kwa makombora vituo na ngome za kijeshi za Israel kaskazini mwa Palestina inayokaliwa kwa mabavu, na kusambaratisha mfumo wa kamera za usalama wa utawala huo haramu.
-
Hizbullah yazima uvamizi wa kijeshi wa Israel kusini ya Lebanon
Jan 22, 2024 03:59Wanajihadi wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon wametibua uvamizi wa kijeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel kusini mwa nchi hiyo ya Kiarabu, huku ngome za utawala huo ghasibu zikiendelea kulengwa kwa makombora ya kundi hilo la muqawama, likiwa ni jibu kwa mauaji ya kimbari yanayoendelea kufanywa na Wazayuni katika Ukanda wa Gaza.
-
Maafisa wa Intelijensia wa Marekani: Israel haitaweza kushinda vita dhidi ya Hizbullah
Jan 08, 2024 02:47Gazeti la Washington Post limeripoti kuwa, tathmini ya siri iliyofanywa na Shirika la Ulinzi wa Intelijensia la Marekani (DIA) imegundua kwamba "itaviwiya vigumu kufanikiwa" vikosi vya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika vita vya medani mbili dhidi ya Hamas huko Gaza na Hizbullah huko Lebanon.
-
Hizbullah yaishambulia Israel kwa makombora 62 katika jibu la kwanza kwa mauaji ya kiongozi wa Hamas
Jan 07, 2024 07:13Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon imesema, imeshambulia kituo cha upelelezi wa angani cha utawala haramu wa Kizayuni wa Israel kwa mlolongo wa makombora katika jibu lake la kwanza kwa mauaji ya Naibu Kiongozi wa Hamas yaliyofanywa na utawala huo wa kigaidi.
-
Hizbullah: Tutaendelea kuishambulia Israel hadi ikomeshe jinai zake Gaza
Dec 13, 2023 07:46Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imesema kundi hilo la muqawama wa Kiislamu litaendelea kufanya mashambulizi ya ulipizaji kisasi dhidi ya Israel, madhali utawala huo wa Kizayuni unaendelea kumwaga damu za Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Hizbullah: Muqawama hautoruhusu Wazayuni wafikie malengo yao Ghaza
Dec 02, 2023 07:09Naibu wa Mkuu wa Baraza la Utendaji la Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amegusia kuanza upya jinai za utawala wa Kizayuni huko Ghaza na kusema kuwa, muqawama kamwe hautowaruhusu Wazayuni kufanikisha malengo yao haramu.
-
Kiongozi wa Hizbullah akutana na maafisa waandamizi wa HAMAS Beirut
Nov 22, 2023 23:37Katibu Mkuu wa Hizbullah jana Jumatano alikutana na ujumbe wa maafisa wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS mjini Beirut kujadili matukio ya Gaza, huku idadi ya wananchi wa Palestina waliouawa shahidi kwenye mashambulizi ya kikatili ya Israel katika eneo hilo linalokaliwa kwa mabavu ikikaribia 15,000.