-
Hizbullah yasema imetumia makombora mapya ya Burkan katika vita na Israel
Nov 12, 2023 03:29Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema wapiganaji wa harakati hiyo ya Muqawama wa Kiislamu wameanza kutumia silaha mpya, likiwemo kombora lenye kichwa kizito katika mapigano yanayoendelea mpakani mwa Lebanon na ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu (Israel), na kuongeza kuwa wataendelea kutumia mpaka huo wenye mvutano kuishinikiza Israel.
-
Sayyid Nasrullah: Machaguo yote dhidi ya Israel yapo mezani
Nov 03, 2023 12:09Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema machaguo yote dhidi ya utawala haramu wa Israel yapo mezani, huku akiuasa utawala huo wa Kizayuni usitishe mara moja uvamizi na mashambulizi yake ya kinyama dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Mapigano ya mpakani yaanza tena kati ya Hizbullah ya Lebanon na utawala wa Kizayuni wa Israel
Nov 02, 2023 09:49Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imejibu jinai zinazoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza kwa kushambulia ngome za jeshi la utawala huo ghasibu.
-
Hizbullah: Ukanda wa Gaza utakuwa kaburi la utawala wa Kizayuni
Oct 21, 2023 23:52Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya nchini Lebanon amesema jinai zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza hazitapita hivi hivi bila kupatiwa jibu na kusisitiza kuwa, eneo hilo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu litageuka na kugeuka na kuwa kaburi la kuuzika utawala huo bandia.
-
Hizbullah yaikosoa Bahrain kwa kuruhusu kufunguliwa ubalozi wa Israel
Sep 06, 2023 07:06Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon imeujia juu utawala wa Aal-Khalifa wa Bahrain kwa kuuruhusu utawala haramu wa Israel kufungua ubalozi wake katika nchi hiyo ya Kiarabu ya Ghuba ya Uajemi.
-
Hizbullah: Utawala wa Kizayuni lazima ufutwe katika eneo
Aug 23, 2023 06:50Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon ameashiria hatari ya utawala wa Kizayuni kwa jamii ya mwanadamu na kusisitiza kuwa, utawala huo haramu unapaswa kufutwa katika uso wa eneo la Asia Magharibi.
-
Utulivu tete katika kambi ya Ain Al-Hilweh kufuatia matamshi ya Sayyid Hassan Nasrullah
Aug 03, 2023 07:38Utulivu wa kiwango fulani umerejea katika kambi ya wakimbizi wa Kipalestina ya Ain Al-Hilweh nchini Lebanon kufuatia matamshi ya Katibu Mkuu wa Hizbullah, Sayyid Hassan Nasrallah, ya kusisitizia ulazima wa kusitishwa mapigano katika kambi hiyo.
-
Jenerali wa Israel akiri; Nasrullah si mtu wa kupuuzwa
Aug 01, 2023 22:49Aliyekuwa Mkuu wa Kitengo cha Operesheni cha jeshi la utawala haramu wa Israel amesema Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon ni shakhsia ambaye hapaswi kupuuzwa.
-
Hizbullah yataka nchi za Waislamu ziwafukuze mabalozi wa Sweden
Jul 21, 2023 04:21Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon ametoa mwito kwa mataifa ya Kiislamu na Kiarabu kuwafukuza mabalozi wa Sweden katika nchi hizo, kulalamikia kitendo cha kuvunjiwa heshima Qurani Tukufu katika nchi hiyo ya Ulaya. Hii ni baada ya mkimbizi wa Iraq aliyeko Sweden kuivunjia heshima Qurani Tukufu kwa kuikanyaga na kuipiga mateke mjini Stockholm jana Alkhamisi.
-
Mifumo ya ulinzi wa anga ya Hizbullah yaitia wahaka Israel
Jul 01, 2023 05:52Gazeti moja la Kiebrania limeripoti kuwa, jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel linatiwa wasi wasi na mifumo ya ulinzi wa anga ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon.