-
Malalamiko ya Sudan kuhusu mashinikizo ya Marekani ya kuwa na uhusiano na Israel
Sep 06, 2020 07:12Serikali ya Trump muda wote imekuwa ikijionesha ni mtumishi asiye na doa wa malengo ya utawala wa Israel na imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kama kuzilazimisha nchi za Kiarabu na za Waislamu kutangaza uhusiano wa kawaida na utawala huo wa Kizayuni. Hata hivyo baadhi ya nchi kama Sudan zimeamua kupinga na pia kukabiliana na njama hizo.
-
Harakati ya PFLP yataka kutimuliwa Imarati katika Jumuiya ya Nchi za Kiarabu
Sep 05, 2020 21:56Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Wananchi kwa ajili ya Ukombozi wa Palestina (PFLP) amesema kuwa, hatua ya Imarati ya kuanzisha uhusiano na utawala haramu wa Israel inakinzana na uamuzi wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu hivyo ametoa wito wa kutimuliwa nchi hiyo sambamba na kurejeshwa Syria katika jumuiya hiyo.
-
Imarati kufungua ubalozi wake Israel ndani ya miezi 5
Sep 05, 2020 06:53Afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Falme za Kiarabu amesema nchi hiyo inatazamiwa kufungua ubalozi ndani ya utawala haramu wa Israel katika kipindi cha kati ya miezi mitatu hadi mitano.
-
Kikao cha kiistratijia cha Beirut, sauti moja ya Wapalestina
Sep 05, 2020 01:53Makundi ya Palestina yameitisha kikao cha pamoja mjini Beirut, Lebanon na kulaani njama mbalimbali zinazofanywa dhidi ya Palestina na wamesisitiza kuwa kitu kimoja na kuendelea na muqawama katika kukabiliana na njama za Kiarabu/Kimagharibi na Kizayuni.
-
Jordan yatoa msimamo kuhusu njama ya UAE na Israel ya kutaka kubadilisha hali ya msikiti wa Al Aqsa
Sep 02, 2020 10:39Wizara ya Mambo ya Nje ya Jordan imetangaza kuwa, Idara ya Waqfu ya nchi hiyo ndio pekee yenye mamlaka na ustahiki wa kusimamia masuala ya Msikiti mtukufu wa Al Aqsa na uendeshaji wake.
-
UN: Muungano wa Saudia ungali unaishambulia Yemen kwa mabomu yaliyopigwa marufuku
Sep 02, 2020 10:35Umoja wa Mataifa umeeleza katika ripoti kuwa, muungano vamizi wa kijeshi unaoongozwa na Saudi Arabia unatumia mabomu yaliyopigwa marufuku ya vishada katika mashambulio yake dhidi ya mji wa al Hudaydah, magharibi mwa Yemen.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi: Imarati imeusaliti Ulimwengu wa Kiislamu na Palestina
Sep 01, 2020 08:40Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameitaja hatua ya serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) ya kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni kuwa ni kuusaliti Ulimwengu wa Kiislamu, Ulimwengu wa Kiarabu na nchi za eneo na kadhia muhimu ya Palestina.
-
Maulamaa wa Kiislamu: Kuwa na uhusiano wa kawaida na Israel ni kudharau jinai zake
Aug 31, 2020 22:02Mkuu wa Umoja wa Kimataifa wa Maulamaa wa Kiislamu amesema kwamba, kitendo cha baadhi ya nchi za Kiarabu cha kuweka uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel ni kufumbia macho jinai za utawala huo katili dhidi ya wananchi wa Palestina.
-
Imarati yazidi kuikumbatia Israel, yaruhusu ndege za utawala huo
Aug 29, 2020 19:28Umoja wa Falme za Kiarabu umebatilisha sheria ya kuususia utawala haramu wa Israel na adhabu ya kukiuka sheria hiyo iliyokuwa imepiga marufuku kufanya miamala yoyote ya kibiashara na kifedha na utawala huo wa Kizayuni.
-
Iran: 'Mashariki ya Kati' mpya itaanzishwa kwa kutimuliwa Marekani katika eneo
Aug 28, 2020 08:05Msaidizi maalumu wa Spika wa Bunge la Iran katika masuala ya kimataifa amesema: 'Mashariki ya Kati' mpya itaundwa baada ya kuhakikisha Marekani imeshatimuliwa kikamilifu katika eneo hili la Asia Magharibi.