-
Wanaharakati wa Imarati wapinga hatua ya serikali ya nchi hiyo ya kufikia mapatano na utawala wa Kizayuni
Aug 20, 2020 19:38Wanaharakati wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) wameyataja mapatano yaliyofikiwa kati ya nchi hiyo na utawala wa Kizayuni ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya pande mbili kuwa ni kukiuka katiba na na kupuuza msimamo wa viongozi wa mwanzo wa Imarati katika kuinga mkono Palestina.
-
Bunge la Tunisia limelaani mapatano kati ya Imarati na utawala wa Kizayuni
Aug 18, 2020 02:27Bunge la Tunisia limelaani mapatano yaliyofikiwa ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia kati ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) na utawala ghasibu wa Israel.
-
Jumuiya ya Maulamaa Algeria: Kuanzisha uhusiano na Israel ni haramu
Aug 17, 2020 08:49Jumuiya ya Maulamaa wa Algeria imesema, ni haramu kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala ghasibu wa Kizayuni wa Israel.
-
Taathira za kiusalama za ‘makubaliano ya usaliti’ ya Israel na Imarati
Aug 17, 2020 02:08Makubaliano ya hiana na usaliti ya Imarati na utawala dhalimu wa Israel ya kuanzisha uhusiano rasmi wa kidiplomasia baina yao yatakuwa na matokeo na taathira tofauti katika uga wa usalama.
-
Mjukuu wa Mandela akosoa mapatano ya kuanzisha uhusiano baina ya Imarati na Israel
Aug 15, 2020 22:41Mjukuu wa shujaa wa mapambano dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi nchini Afrika Kusini amekosoa mapatano ya kuanzishwa uhusiano wa kidiplomasia baina ya Imarati na utawala haramu wa Israel.
-
UAE: Hakuna hakikisho lolote la kughairishwa umegaji wa eneo la Ufukwe wa Magharibi
Aug 15, 2020 21:46Waziri wa Nchi katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Imarati (UAE) amekiri kuwa hakuna hakikisho lolote lililotolewa katika makubaliano kati ya nchi hiyo na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel la kufutwa mpango wa kulimega eneo la ardhi ya Palestina la Ufukwe wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Spika wa Bunge la Iran: Imarati imejidhalilisha kwa kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni
Aug 14, 2020 22:29Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa makubaliano ya Imarati na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuanzisha uhusiano baina ya pande hizo mbili ni ya kijidhalilisha na ni usaliti kwa thamani za Umma wa Kiislamu na malengo ya taifa la Palestina.
-
Muungano wa Maulama wa Kiislamu: Hatua ya Imarati kuanzisha uhusiano na Israel ni usaliti mkubwa
Aug 14, 2020 22:28Jumuiya ya Muungano wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Kiislamu imelaani makubaliano ya kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia baina ya Imarati na utawala haramu wa Israel yaliyofikiwa kwa upatanishi wa Marekani.
-
Palestina yamrejesha nyumbani balozi wake Abu Dhabi baada ya Imarati kuanzisha uhusiano na Israel
Aug 14, 2020 05:04Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Serikali ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina ametangaza kuwa balozi wa Palestina mjini Abu Dhabi ameitwa nyumbani kulalamikia hatua ya Imarati ya kuanzisha rasmi uhusiano wa kidiplomasia na utawala haramu wa Israel.
-
Mapatano ya aibu na usaliti kati ya Imarati na utawala wa Kizayuni
Aug 14, 2020 04:29Umoja wa Falme za Kiarabu yaani Imarati, utawala ghasibu wa Israel na Marekani zimetoa taarifa ya pamoja zikitangaza kwamba Imarati na utawala haramu wa Israel zimefikia mapatano ya kuanzisha uhusiano wa kawaida baina yazo.