-
Radiamali ya Iran, China kwa safari ya Pelosi katika kisiwa cha Taiwan
Aug 03, 2022 07:44Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekosoa safari ya Nancy Pelosi, Spika wa Kongresi ya Marekani katika kisiwa cha Taiwan na kubainisha kuwa, ziara hiyo ni muendelezo wa mienendo ya kichokozi na kichokezi ya Washington.
-
China yaitaka Marekani iiondolee Iran vikwazo haramu
Aug 03, 2022 07:27Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Kudhibiti Silaha katika Wizara ya Mambo ya China ameitaka Marekani iiondolee Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vikwazo haramu.
-
Kani: Iran iko tayari kuipa Marekani fursa nyingine ya kujirudi
Jul 31, 2022 22:17Kiongozi wa timu ya Iran katika mazungumzo ya nyuklia ya Vienna amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ipo tayari kutamatisha mazungumzo ya kuiondolea vikwazo Tehran haraka iwezekanavyo, sanjari na kuipa Marekani fursa nyingine ya kurekebisha makosa yake.
-
Raisi: Mahudhurio ya wananchi katika medani ndio nguzo kuu ya nguvu na usalama wa taifa
Jul 28, 2022 10:30Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kwamba mahudhurio na kushiriki wananchi katika nyanja mbalimbali za maendeleo ya taifa ndio sehemu muhimu zaidi ya nguvu ya kitaifa na usalama wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Abdollahian: Iran iko tayari kuitatulia dunia mgogoro wa nishati
Jul 27, 2022 21:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu ipo tayari kukidhi mahitaji ya nishati ya jamii ya kimataifa.
-
Karibuni hivi Ugiriki itarejesha shehena ya mafuta ya Iran iliyoiba
Jul 26, 2022 22:32Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Ugiriki umetangaza kuwa operesheni ya kuyahamisha na kuyarejesha mafuta ya Iran yaliyoibwa itaanza hivi karibuni.
-
"Marekani ikiwa na irada ya kisiasa kama Iran, makubaliano yatafikiwa"
Jul 25, 2022 06:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu haitakubali kushinikizwa juu ya kufikia haraka muafaka wa kujaribu kuhuisha makubaliano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Iran yavunja mtandao wa majasusi wa Mossad ya Israel
Jul 24, 2022 03:14Wizara ya Intelijensia ya Iran imetangaza habari ya kutiwa mbaroni majasusi kadhaa waliokuwa wakitumikia shirika la ujasusi la Israel (Mossad).
-
Mazungumzo kati ya marais wa Iran na Ufaransa; Raisi akosoa sera za kuzusha migogoro za Wamagharibi
Jul 24, 2022 03:04Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, zzimio lililotolewa na Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki dhidi ya Iran ni hatua ya kuzusha mgogoro iliyokuwa na lengo la kuliwekea mashinikizo taifa la Iran.
-
Raisi: Azimio la IAEA dhidi ya Iran lilitia doa muamana wa kisiasa
Jul 23, 2022 22:57Rais wa Iran amesema azimio dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu katika Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) lilikuwa na taathira hasi kwa muamana na irada ya kisiasa ya pande husika.