-
Iran yazindua mfumo wa makombora wa Khordad 15 + Video
Jun 09, 2019 09:26Iran imezindua mfumo wa kujilinda kwa makombora uliotengenezwa kikamilifu hapa nchini unaoweza kulenga shabaha sita za adui kwa wakati mmoja.
-
Heiko Maas : Nchi za Ulaya zinafungamana na mapatano ya nyuklia ya Iran
Jun 08, 2019 23:06Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Heiko Maas amekutana na Waziri Mkuu wa Iraq Adel Abdul Mahdi mjini Baghdad siku ya Jumamosi na kusema nchi za Umoja wa Ulaya zinafungamana na mapatano ya nyuklia ya Iran maarufu kama JCPOA.
-
Russia: Madai kuwa Iran ilituomba tuiuzie ngao ya S-400 ni uvumi mtupu
Jun 07, 2019 21:47Naibu Waziri Mkuu wa Russia katika Masuala ya Ulinzi amesema kwamba, Moscow haijapata ombi kutoka Iran la kuiuzia ngao ya makombora ya S-400.
-
Ayatullah Kashani: Katu Iran haitasaimu amri mbele ya njama za adui
Jun 07, 2019 08:36Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa mjini Tehran amesema katu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitasalimu amri mkabala wa njama za maadui na kusisitiza kwamba taifa hili litaendelea kufungamana na muqawama.
-
Iran yakosoa matamshi ya Rais wa Ufaransa alipokutana na Trump
Jun 07, 2019 02:58Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amejibu matamshi ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa alipokutana na mwenzake wa Marekani mjini Paris na kusema matamshi ya Macron hayasaidii katika kulindwa mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Siasa za pamoja za Iran na Qatar; uimarishaji wa usalama wa eneo
Jun 06, 2019 04:01Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kwamba Iran inataka kuimarisha usalama wa eneo zima la Asia Magharibi na kwamba haina nia ya kuanzisha mapigano na nchi yoyote ile. Hata hivyo ameongeza kuwa iwapo Iran itashambuliwa na nchi yoyote katika eneo basi nchi hiyo itapata jibu la kuifanya ijute ni kwa nini ilianzisha mashambulizi.
-
Russia na China zalaani vikwazo vya upande mmoja vya Marekani dhidi ya Iran
Jun 06, 2019 03:19Marais wa Russia na China sanjari na kulaani vikwazo vya upande mmoja vya Marekani dhidi ya Iran, lakini pia wamezitaka pande husika kufungamana na makubaliano ya nyuklia ya Vienna yanayojulikana kama JCPOA.
-
Zarif aikosoa Mossad ya Israel kwa kuituhumu Iran kwa ulipuaji wa meli za mafuta al-Fujairah, UAE
Jun 05, 2019 22:45Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amepuuzilia mbali 'taarifa za kiintelijensia' za Shirika la Kijasusi la Utawala wa Kizayuni wa Israel Mossad zinazodai kwamba Iran imehusika na kulipuliwa meli za mafuta katika Bandari ya al-Fujairah huko Umoja wa Falme za Kiarabu, akisisitiza kuwa amewahi kutoa indhari huko nyuma kuhusu kupikwa njama za kutaka kuibua taharuki katika eneo.
-
Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu; 'Muqawama (ukakamavu)', siri ya ushindi dhidi ya adui
Jun 05, 2019 22:01Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amewaambia viongozi na wananchi wa Iran kutohadaika na ujanja wa kisiasa wa rais wa Marekani.
-
Alkhamisi, tarehe 6 Juni, 2019
Jun 05, 2019 21:53Leo ni Alkhamisi tarehe 6 Juni mwaka 2019.