-
Afisa wa zamani wa CIA: Saudia na Israel zinataka kuiburuza Marekani kwenye vita dhidi ya Iran
Nov 14, 2017 13:18Mtaalamu wa zamani wa kitengo cha kupambana na ugaidi aliyekuwa pia afisa wa intelijinsia ya kijeshi wa Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) amesema utawala wa Kizayuni wa Israel na Saudi Arabia hazina uwezo wa kuishinda kijeshi Iran hivyo zinajaribu kuiburuza Marekani kwenye vita dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Iran yaishukuru Jamii ya Kimataifa; Zarif: Iran ina uwezo wa kusimamia maafa ya zilzala
Nov 14, 2017 03:16Muhammad Javad Zarif, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran leo asubuhi ametoa shukrani kufuatia salamu za pole zilizotolewa kutoka maeneo mbalimbali baada ya kujiri tetemeko la ardhi magharibi mwa Iran na kufuatia pendekezo la nchi mbalimbali za kutaka kuwasaidia waathirika wa zilzala hiyo na akasema kuwa: Iran hivi sasa ina uwezo wa kushughulikia mgogoro huo wa tetemeko la ardhi kwa kustafidi na suhula za ndani.
-
Iran: Ripoti mpya ya IAEA inakinzana na madai hewa ya Marekani kuhusu JCPOA
Nov 14, 2017 01:09Balozi wa Iran katika Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia (IAEA) amesema ripoti ya hivi punde ya wakala huo sanjari na kuthibitisha kuwa Tehran imefungamana na makubaliano ya nyuklia ya Vienna, lakini pia imekinzana na tuhuma zisizo na msingi zilizotolewa na Washington kuhusu mapatano hayo ya kimataifa.
-
Mtetemeko mkubwa wa ardhi katika mpaka wa Iran na Iraq katika Picha
Nov 13, 2017 13:06Hadi tunapokea habari hii, idadi ya watu waliokuwa wamepoteza maisha yao kutokana na mtetemeko mkubwa wa ardhi uliopita eneo la mpakani mwa Iran na Iraq ilikuwa imeshafikia watu 445 na wengine 7100 kujeruhiwa.
-
Qatar: Tutaimarisha na kulinda uhusiano wetu na Iran
Nov 13, 2017 11:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Qatar amesema kuwa, Iran ni nchi jirani na nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi na kwamba Doha ina manufaa ya pamoja na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran hivyo haiwezi kukata uhusiano wake na Tehran.
-
Mwanga wa kuzidi kuimarika uhusiano wa Ulaya na Iran
Nov 13, 2017 09:12Is'haq Jahangiri, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametangaza habari ya kuwekwa kwenye ajenda kuu suala la kufunguliwa ofisi ya Umoja wa Ulaya hapa mjini Tehran.
-
Ulimwengu wa Spoti, Nov 13
Nov 13, 2017 04:01Hujambo mpenzi msikilizaji wa RT na hususan ashiki wa spoti na karibu tutupie jicho matukio mawili matatu ya michezo yaliyogonga vichwa vya habari ndani na nje ya nchi katika kipindi cha siku saba zilizopita, karibu..
-
Iran yakadhibisha 'madai ya kitoto' ya Bahrain kuhusu kushambuliwa bomba la mafuta
Nov 13, 2017 00:49Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekanusha kile ilichokitaja kama 'madai ya kitoto' yaliyotolewa na Bahrain dhidi yake.
-
Yemen: Madai ya Marekani kuwa Iran imehusika katika shambulizi la Riyadh ni kichekesho
Nov 11, 2017 12:18Wizara ya Mambo ya Nje ya Yemen imekadhibisha madai ya Marekani kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ilihusika katika shambulizi la kombora la Burkan 2 kutoka Yemen kwenda Riyadh na imeyataja madai hayo kuwa ni kichekesho.
-
Mamilioni katika maombolezo ya Arubaini ya Imam Hussein AS
Nov 08, 2017 23:40Leo mamilioni ya watu wanashiriki katika maombolezo kwa munasaba wa Arubaini ya Mjukuu wa Mtume Muhammad SAW, Imam Hussein AS.