-
Iran: Vikwazo vipya vya Marekani ni ‘ugaidi wa kiuchumi’ na ‘uhalifu dhidi ya ubinadamu’
Aug 21, 2026 10:34Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani vikali mzunguko mpya wa vikwazo vya kiuchumi vilivyowekwa na Marekani dhidi ya taifa hili, ikisisitiza kuwa hatua hizo ni sawa na “ugaidi wa kiuchumi” na “uhalifu dhidi ya ubinadamu.”
-
Araghchi: “Ugaidi wa kiuchumi” wa Trump dhidi ya Iran ni mbinu ya kupotosha umma kuhusu matatizo ya uchumi wa Marekani
Aug 21, 2026 06:13Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ameionya Marekani kwamba kuendeleza sera “zilizoshindwa” dhidi ya Iran kutasababisha kurudi nyuma zaidi kwa Washington. Kauli hiyo imekuja huku Marekani ikigeukia mashinikizo ya kiuchumi baada ya kukiri kushindwa katika uchokozi wake wa kijeshi dhidi ya Iran.
-
Iran yamtahadharisha Trump kuhusu 'fikra potofu' ya kudai Mlango-Bahari wa Hormuz ni eneo la Marekani
Aug 19, 2026 04:16Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayeshughulikia Masuala ya Kisheria na Kimataifa Kazem Gharibabadi amemkosoa vikali Rais Donald Trump wa Marekani kwa madai yake kuhusu Lango la Bahari la Hormuz, akionya kuwa "fikra yake potofu" ya kuihesabu njia hiyo muhimu ya maji kama "eneo jipya la Marekani" inapasa kurekebishwa, la sivyo Tehran itamweka sawa.
-
Pezeshkian: Ustahimilivu, umoja, na matumaini ni nguzo ya Iran kukabiliana na vitisho vya nje
Aug 18, 2026 11:43Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema vita vya Iraq dhidi ya Iran, vinavyofahamika nchini Iran kama Vita vya Kujihami Kutakatifu, vina somo muhimu ambalo ni ustahimilivu, umoja, na matumaini.
-
Qalibaf: Iran italipiza kisasi damu ya Kiongozi Shahidi
Aug 18, 2026 11:41Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, ameahidi kwamba Jamhuri ya Kiislamu haitaruhusu damu ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi, Ayatollah Sayyid Ali Khamenei, na mashahidi wengine wa uvamizi wa Marekani na Israel dhidi ya taifa hili “kupotea bila kulipiziwa kisasi.”
-
Kamanda: Iran ilitungua ndege zaidi ya 200 za adui katika Uvamizi wa Marekani na Israel
Aug 18, 2026 11:38Naibu Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema kuwa mifumo ya ulinzi wa anga ya Iran ilitungua ndege za adui zaidi ya 200, zikiwemo ndege zisizo na rubani (drones) na ndege zenye marubani, wakati wa uvamizi wa hivi karibuni wa Marekani na Israel.
-
Iran yaonyesha mabaki ya ndege za kivita za Marekani na Israel ilizozitungua +Video
Aug 15, 2026 03:54Iran imeonyesha sehemu za vifaa vilivyopatikana kutoka ndege za kivita zisizo na rubani (droni) za Marekani na Israel, pamoja na ndege ya kivita ya F-15 ambazo zilitunguliwa kwa mifumo ya ulinzi ya Iran wakati wa vita. Mifumo ya ulinzi iliyotumika kutungua ndege hizo za adui imeundwa hapa nchini.
-
Rezaei: Mlango-Bahari wa Hormuz utafunguliwa ikiwa tu US itayakubali masharti ya Iran
Aug 12, 2026 12:33Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema, kufunguliwa tena kikamilifu Mlango-Bahari wa Hormuz katika Ghuba ya Uajemi, ambao umewekewa vizuizi vya uvukaji na Iran tangu mwanzoni mwa mwezi Machi kutokana na uchokozi wa kijeshi wa Marekani na utawala wa kizayuni wa Israel kutafanyika pale tu Marekani itakapoyakubali masharti ya Iran.
-
Shambulio la kinyama la US kisiwani Qeshm, Iran laua wazazi na mtoto wao mdogo
Jul 30, 2026 11:09Wanafamilia watatu, wakiwemo mama, baba na mtoto wao wa kiume wa miaka miwili, wameuawa shahidi katika shambulio la kinyama la anga la jeshi la kigaidi la Marekani lililolenga jengo la makazi kwenye Kisiwa cha Qeshm kusini mwa Iran.
-
Pezeshkian: Uharibifu wa miundombinu uliosababishwa na Marekani ufuatiliwe kisheria kimataifa
Jul 27, 2026 03:57Rais Masoud Pezeshkian amelaani mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani dhidi ya miundombinu ya usafiri ya Iran akiyataja kuwa ni "uhalifu wa kivita," na kutaka hatua za kisheria za kimataifa zichukuliwe dhidi ya uharibifu uliosababishwa na nchi hiyo kwenye vituo vya mpakani, vituo vya forodha na mitandao ya usafirishaji.