-
Hashdu sh-Sha'abi yaonya juu ya njama za Marekani za kuwaingiza Iraq magaidi wa Daesh
Sep 24, 2018 22:54Msemaji wa kamandi ya upande wa kaskazini ya Harakati ya Wananchi ya Hashdu sh-Sha'abi ya nchini Iraq ameonya juu ya njama za Marekani za kuwasaidia magaidi wa genge la Daesh (ISIS) kutoka Idlib, Syria kuingia nchini humo.
-
Marekani yatuma wanajeshi wake katika mpaka wa Iraq na Syria
Sep 21, 2018 23:34Duru za Iraq zimearifu kuwa Marekani imetuma wanajeshi wake karibu na kivuko cha al Qaim katika mpaka wa Iraq na Syria.
-
Wabunge wa Kisuni Iraq: Marekani inatushinikiza tumteue tena Haider al-Abadi kuwa Waziri Mkuu
Sep 20, 2018 10:53Mjumbe wa Mrengo wa Ujenzi wa Iraq ambaye pia ni mbunge wa Kisuni katika Bunge la nchi hiyo amefichua kuwa serikali ya Marekani inawashinikiza wabunge wote wa Kisuni nchini Iraq wamuungE mkono Haider al-Abadi ili ateuliwe tena kuwa waziri mkuu.
-
Iran: Madai ya US dhidi yetu kuhusu Basra hayana msingi
Sep 12, 2018 22:09Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema madai ya Marekani kwamba Tehran imehusika katika machafuko ya mji wa Basra nchini Iraq ni ya kipuuzi, ya kichochezi na yasiyokuwa na msingi.
-
Sisitizo la Ibrahim Jaafari la kuondoka wanajeshi wa Uturuki huko Iraq
Sep 12, 2018 03:15Ibrahim Jaafari Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq amesisitiza kuondoka haraka iwezekanavyo wanajeshi wa Uturuki katika ardhi ya nchi hiyo.
-
Hashdu Sha'abi: Marekani ndio inayochochea ghasia Basra, Iraq
Sep 09, 2018 02:42Kamanda wa ngazi za juu wa kikosi cha kujitolea cha wananchi nchini Iraq cha Hashdu Sha'abi amesema harkati hiyo ya wananchi tayari imewakabidhi maafisa wa serikali ya Baghdad ushahidi unaoonesha kuwa ubalozi mdogo wa Marekani mjini Basra ndio uliohusika katika kuratibu na kuchochea machafuko yanayoendelea kushuhudiwa hivi sasa katika mkoa wa Basra, kusini mwa nchi hiyo ya Kiarabu.
-
Waziri Mkuu wa Iraq: Malalamiko ya wananchi wa Basra ni ya haki
Sep 08, 2018 10:03Waziri Mkuu wa Iraq amesema kuwa, anakubaliana na mpango wa kuungalia mkoa wa Basra kwa mtazamo maalumu katika baadhi ya vipengee vinavyohusiana na utekelezaji wa bajeti na maamuzi ya serikali.
-
Kundi la Asa'ib Ahl al-Haq: Wanaofanya ghasia mkoa wa Basra, Iraq wanatekeleza malengo ya Marekani
Sep 08, 2018 02:44Katibu Mkuu wa kundi la Asa'ib Ahl al-Haq ambalo ni sehemu ya Harakati ya Wananchi ya Hashdu sh-Sha'abi nchini Iraq, amesema kuwa watu wanaofanya ghasia katika mkoa wa Basra, wanatekeleza malengo maalumu kupitia maandamano.
-
Mahakama Iraq yawafunga maisha jela magaidi wa ISIS
Sep 02, 2018 22:12Mahakama nchini Iraq imewafunga kifungo cha maisha gerezani watu wanne ambao wamepatikana na hatia ya kujiunga na kundi la magaidi wakufurishaji wa ISIS au Daesh.
-
Kuendelea kupingwa uingiliaji wa Marekani katika mchakato wa kuundwa serikali mpya nchini Iraq
Aug 31, 2018 02:01Kongresi ya Taifa ya Iraq imesisitiza kuwa, uingilkiaji wa Marekani katika suala la kuundwa serikali mpya ya nchi hiyo umezidi kuvuruga hali ya kisiasa na kuzidi kuufanya tata mwenendo wa kisiasa wa Iraq.