-
Marekani na washirika wake wakiri, wameua mamia ya raia Iraq na Syria
Oct 27, 2017 01:17Marekani na washirika wake katika kile kinachodaiwa ni muungano wa kupambana na Daesh wamekiri kwamba, wameua raia wengine wasiopungua 51 wasio na hatia katika nchi za Syria na Iraq, suala linaloopandisha juu idadi ya raia waliouawa na muungano huo na kufikia watu 786.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Siri ya ushindi wa karibuni Iraq ni umoja na uungaji mkono wa vijana waumini na mashujaa
Oct 26, 2017 13:04Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullahil-Udhma Sayyid Ali Khamenei amesema, umoja wa kaumu tofauti na uungaji mkono wa serikali ya Iraq kwa vikosi vya wananchi na vijana waumini na mashujaa wa nchi hiyo ndio siri ya ushindi uliopatikana karibuni dhidi ya magaidi na waungaji mkono wao.
-
Kamanda wa jeshi la Marekani: Tillerson hajui chochote kuhusu masuala ya Iraq
Oct 24, 2017 10:28Kamanda wa zamani wa jeshi la Marekani nchini Iraq, Mark Hertling amesema kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa nchi hiyo Rex W. Tillerson, hana ufahamu kuhusiana na masuala magumu ya Iraq.
-
Malaysia yasema magaidi 34 wa nchi hiyo wameangamizwa Iraq na Syria
Oct 24, 2017 01:00Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani wa Malaysia amesema kuwa, kwa akali magaidi 34 wenye uraia wa taifa hilo wameangamizwa nchini Iraq na Syria.
-
Al-Abadi: Iraq itaendelea kuwa moja iliyoungana na yenye uthabiti
Oct 19, 2017 12:43Waziri Mkuu wa Iraq Haidar Al Abadi ametangaza kuwa nchi hiyo itabaki kuwa moja na kwamba Iraq yenye uthabiti ni bora kwa uthabiti wa eneo la Mashariki ya Kati na dunia kwa jumla.
-
Nouri al-Maliki: Operesheni ya kuidhibi Kirkuk ni kulinda umoja wa kitaifa wa Iraq
Oct 17, 2017 05:06Nouri al-Maliki, Makamu wa Rais wa Iraq amesema kuwa operesheni za jeshi la serikali za kuudhibiti mji wa Kirkuk, hazikuwa dhidi ya raia wa Kikurdi bali zilikuwa dhidi ya wale wanaokiuka katiba na sheria za Iraq.
-
Wairaq washerehekea kufurushwa Wakurdi kutoka Kirkuk, al-Abad aamuru kupeperushwa bendera ya Iraq
Oct 16, 2017 13:07Wakazi wa mji wa Kirkuk nchini Iraq wamemiminika katika barabara za mji huo kushangilia ushindi wa jeshi la serikali kwa kushirikiana na harakati ya wananchi ya Hashdu sh-Sha'abi kwa hatua ya kuwafurusha wapiganaji wa Kikurdi mjini hapo na kisha kudhibiti hali ya mambo.
-
Siku za kundi la kigaidi la Daesh nchini Iraq zaanza kuhesabika
Oct 11, 2017 23:16Sambamba na ushindi wa kila siku wa jeshi la Iraq na makundi ya kujitolea ya wananchi katika mapambano ya kuliangamiza kundi la kigaidi la ِِِDaesh na kusafisha kabisa maeneo yote ya nchi hiyo, Waziri Mkuu wa Iraq, Haider al-Abadi ametangaza kuwa, kundi hilo litashindwa kikamilifu hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu.
-
Serikali ya Iraq yapitisha vikwazo vipya dhidi ya eneo la Kurdistan
Oct 09, 2017 23:37Katika kujibu hatua ya viongozi wa eneo la Kurdistan ya Iraq ya kukiuka katiba na kuitisha kura ya maoni ya kutaka kujitenga na kujitangazia uhuru, serikali kuu ya Iraq imechukua maamuzi mapya ya kuliadhibu eneo hilo.
-
Iraq kuwahukumu wanachama wa ISIS, raia wa Ulaya
Oct 08, 2017 10:42Vyombo vya mahakama nchini Iraq vinatazamiwa kuwatolea hukumu ikiwemo hukumu ya kifo, makumi ya wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh (ISIS) raia wa nchi za Ulaya.