-
UN yaunga mkono kutambuliwa Siku ya Nakba ya Wapalestina
Dec 01, 2022 09:46Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limepiga kura ya kuunga mkono azimio lenye maslahi kwa Palestina la kutaka kuadhimishwa Siku ya Nakba, inayokumbusha tukio chungu la kuasisiwa utawala bandia na haramu wa Israel mwaka 1948.
-
Kanali ya Kizayuni: Israel inakabiliwa na Intifadha mpya ya Wapalestina
Nov 30, 2022 07:15Chombo kimoja cha habari cha Kizayuni kimesema hali ya usalama katika eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan linalokaliwa kwa mabavu ni ya 'hatari' na kwamba Tel Aviv inakabiliwa na Intifadha mpya ya Wapalestina.
-
Uingereza yasisitiza haitauhamishia ubalozi wake Quds
Nov 22, 2022 04:06Kwa mara nyingine, Uingereza kutokana na mashinikizio na ukosoaji wa ndani na nje ya nchi, imesisitiza kuwa haina mpango wa kuuhamishia ubalozi wake katika mji wa Quds tukufu, huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Kombe la Dunia; Vijana wa Kiarabu wakataa kuzungumza na wanahabari wa Israel
Nov 21, 2022 07:55Mashabiki wa soka wa nchi za Kiarabu wamekataa kuzungumza na waandishi wa habari wa mashirika ya utawala haramu wa Israel nchini Qatar, kunakofanyika fainali za Kombe la Dunia za mwaka huu 2022; kuonyesha upinzani wao wa kuanzishwa uhusiano wa kawaida na utawala huo bandia unaokalia kwa mabavu ardhi za Palestina.
-
Israel yatumia bunduki za roboti dhidi ya Wapalestina Ukingo wa Magharibi
Nov 17, 2022 03:25Jeshi la utawala haramu wa Israel limepeleka silaha mpya za roboti katika eneo la Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan, huku makabiliano baina ya Wazayuni na Wapalestina yakipamba moto.
-
Mrithi wa Ufalme Bahrain apewa mwaliko na Netanyahu
Nov 14, 2022 07:27Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa zamani wa Israel anayetazamiwa kuunda serikali mpya ya utawala wa Kizayuni amemualika Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Bahrain, Salman bin Hamad Aal Khalifah kuitembelea ardhi ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu na kupachikwa jina la Israel.
-
Kuwait: Israel inapaswa kuweka vituo vyake vya nyuklia chini ya usimamizi wa IAEA
Nov 12, 2022 04:04Kwa mara nyingine tena Kuwait imeutaka utawala haramu wa Israel ujiunge na Mkataba wa Kuzuia Usambazaji wa Silaha za Nyuklia (NPT) na kuweka vituo vyake vyote vya nyuklia chini ya mfumo wa usimamizi wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).
-
Makampuni ya Oman na Kuwait yajiondoa kwenye maonyesho ya Bahrain kuisusia Israel
Nov 04, 2022 03:14Shirika la ndege la bei nafuu la Oman na Benki ya Kiislamu ya Kuwait zimeamua kujiondoa katika maonyesho yajayo ya Kimataifa ya Anga ya Bahrain (BIAS) baada ya kubaini wajumbe kutoka makampuni ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel watashiriki katika maonyesho hayo, ikiwa ni hatua ya kuonyesha mshikamano na uungaji mkono kwa Palestina.
-
HAMAS: Wapalestina wataendeleza mapambano ya ukombozi
Nov 03, 2022 08:10Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imesema wananchi wa Palestina wataendeleza kwa nguvu zote jitihada na mapambano ya kulikomboa kikamilifu taifa lao kutoka kwenye makucha ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Uchaguzi wa tano wa bunge la Israel katika muda wa chini ya miaka minne
Nov 02, 2022 04:50Uchaguzi wa tano wa bunge la Israel katika muda wa chini ya miaka minne ulifanyika jana Jumanne tarehe 1 Novemba.