-
Indhari ya Wazayuni kuhusu kusambaratika uchumi wa Israel
Nov 11, 2020 04:47Naftali Bennett, kiongozi wa chama cha harakati ya mrengo wa kulia wenye kufurutu ada kinachojulikana kama chama cha The New Right amesema kuwa, katika hali ya hivi sasa Israel inaelekea upande hatari na wa kutisha na kwamba, imo mbioni kusambaratika kiuchumi.
-
Jumamosi, 7 Novemba, 2020
Nov 07, 2020 04:05Leo ni Jumamosi tarehe 21 Mfunguo Sita Rabiul Awwal 1442 Hijria sawana tarehe 7 Novemba 2020 Miladia.
-
Malawi kuwa nchi ya kwanza ya Afrika kufungua ubalozi Quds inayokaliwa kwa mabavu
Nov 05, 2020 00:27Malawi inatazamiwa kuwa nchi ya kwanza ya Afrika kufuata mkumbo wa Marekani wa kufungua ubalozi katika mji mtukufu wa Quds huko Palestina unaokaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Israel.
-
Tahadhari ya kutokea tetemeko la kisiasa katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu Palestina
Nov 03, 2020 03:31Kwa kuendelea maandamano katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na utawala dhalimu wa Israel, rais wa utawala huo ametoa tahadhari kuhusu mgogoro mkubwa na hatari ambao amekiri kwamba tayari umeanza kutetemesha kuta za utawala huo.
-
Iran: Njama mpya za Marekani na Israel dhidi yetu zitafeli
Oct 28, 2020 04:15Katibu wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema njama mpya za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel za kutaka kutoa pigo kwa Iran kupitia uanzishwaji wa uhusiano wa kawaida na Tel Aviv, zitagonga mwamba.
-
Al Burhan: Bunge la Sudan linaweza kubadilisha uamuzi kuhusu makubaliano tuliyofikia na Israel
Oct 27, 2020 04:20Kiongozi wa baraza la utawala la Sudan ametetea makubaliano ya kuaibisha iliyofikia serikali ya mpito ya nchi hiyo na Israel na kudai kuwa bunge la Sudan linaweza kuupitia upya uamuzi huo wa kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni.
-
Mamlaka ya Ndani ya Palestina: Baitul Muqaddas haitauzwa, si kwa amri ya Israel wala Marekani
Oct 27, 2020 03:54Msemaji wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesisitiza kuwa Quds tukufu haitauzwa, si kwa amri ya Israel, serikali ya Marekani wala nchi nyingine yoyote duniani.
-
Lawama na ukosoaji dhidi ya Marekani kwa kuyatuhumu mashirika matatu ya haki za binadamu kuwa eti yana chuki na Mayahudi
Oct 23, 2020 09:42Katika kipindi cha miaka minne ya utawala wake, Rais Donald Trump wa Marekani amechukua hatua nyingi kwa madhumuni ya kuitetea na kuiunga mkono Israel na kuyapiga vita mashirika ya kimataifa ambayo yamechukua msimamo wa kuwatetea na kuwaunga mkono wananchi madhulumu wa Palestina dhidi ya jinai wanazofanyiwa na utawala huo wa Kizayuni.
-
Afisa wa Sudan: Nchi inakaribia kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni
Oct 22, 2020 23:31Afisa mmoja wa Sudan ambaye hakutaka jina lake litajwe amedai kuwa muda wa nchi hiyo kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel umekaribia licha ya vyama mbalimbali na wananchi kupinga jambo hilo.
-
Wazayuni waliofilisika kwa corona waongezeka kwa asilimia 40
Oct 22, 2020 08:51Kuenea maambukizi ya kirusi cha corona katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na ambazo zimepachikwa jina bandia la Israel, kumekuwa na madhara makubwa kwa uchumi wa utawala wa Kizayuni na sasa hivi Wazayuni waliofilisika kutokana na ugonjwa huo hatari wameongezeka kwa asilimia 40.