-
Nyaraka za jeshi la Israel zafichua: Mfungwa wa Kipalestina aliyebakwa alikuwa raia, si mpiganaji
Nov 04, 2025 07:48Waraka wa siri wa jeshi la Israel umefichua kwamba mtu aliyeshambuliwa kikatili na kubakwa na kundi la wanajeshi wa Israel katika gereza maarufu la Sde Teiman mnamo Julai mwaka jana hajawahi kushtakiwa kwa uhalifu wowote na alikuwa raia, kinyume na madai kwamba alikuwa na mwanachama harakati za mapambano ya Hamas.
-
Israel yaandaa muswada wa 'kifashisti' wa kuruhusu utoaji wa hukumu ya adhabu ya kifo kwa Wapalestina
Nov 03, 2025 22:55Kamati moja ya wabunge wa utawala wa kizayuni wa Israel imeidhinisha muswada wa kuanzisha utoaji wa adhabu ya kifo kwa Wapalestina wanaoshikiliwa kwenye magereza ya utawala huo, na kufungua njia ya kusomwa hoja hiyo kwa mara ya kwanza bungeni licha ya kuandamwa na lawama nyingi.
-
Israel yaendelea kuwatesa kwa njaa Wapalestina kwa kuruhusu 24% tu ya misaada kuingizwa Ghaza
Nov 02, 2025 03:20Mamlaka za Palestina katika Ukanda wa Ghaza zimetangaza kuwa utawala wa kizayuni wa Israel umeruhusu kuingizwa katika eneo hilo sehemu ndogo tu ya misaada ya kibinadamu kinyume na ilivyoafikiwa katika makubaliano ya usitishaji mapigano yanayosimamiwa na serikali ya Marekani, ambayo yalianza kutekelezwa mwezi uliopita.
-
Israel yaendelea kukiuka makubaliano na Lebanon, yashambulia na kuua watu 4 na kujeruhi 3
Nov 02, 2025 02:57Shambulio la anga lililofanywa na jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel limesababisha vifo vya watu wanne na kuwajeruhi wengine watatu kusini mwa Lebanon ukiwa ni mwendelezo wa mashambulizi ya kigaidi yanayofanywa na Tel Aviv ndani ya ardhi ya nchi hiyo, ambayo yanakiuka makubaliano ya kusitisha mapigano yaliyofikiwa mwishoni mwa Novemba 2024 kati ya Harakati ya Muqawama ya Hizbullah na utawala huo ghasibu.
-
Jinsi himaya isiyo na masharti ya Ujerumani kwa Israel inavyoakisi unafiki wa vigezo vya Magharibi vya haki za binadamu
Nov 01, 2025 08:59Msemaji wa harakati ya Hamas amekosoa kauli za Kansela wa Ujerumani Friedrich Mertz za kujaribu kutetea uhalifu na jinai za utawala haramu wa Israel dhidi ya watu wa Palestina.
-
Israel yashambulia kusini mwa Lebanon; raia mmoja auawa
Oct 30, 2025 08:54Wanajeshi wa Israel wamefanya shambulizi la nchi kavu katika mkoa wa kusini mwa Lebanon wa Nabatieh, huo ukiwa ukiukaji mwingine wa makubaliano ya kusitisha mapigano ambayo yalianza kutekelezwa karibu mwaka mmoja uliopita.
-
Marufuku ya kuingia wanariadha wa utawala wa Kizayuni nchini Indonesia
Oct 27, 2025 01:00Indonesia inachukulia marufuku ya kuingia wanariadha wa utawala Kizayuni wa Israel katika nchi hiyo kuwa haki yake halali.
-
Ni mambo gani yameifanya Israel itengwe kisiasa na kijamii kiasi hiki?
Oct 23, 2025 23:02Israel inakabiliwa na mgogoro mkubwa zaidi wa kisiasa katika historia yake. Yair Lapid, kiongozi wa upinzani wa utawala wa Kizayuni, alikiri hivi karibuni katika kikao cha kamati moja ya Knesset kwamba Israel hivi sasa iko katika mgogoro mkubwa zaidi wa kisiasa katika historia yake.
-
Unafiki wa Ulaya mkabala wa Gaza: Biashara na Israel au kuheshimu haki za binadamu?
Oct 22, 2025 22:59Umoja wa Ulaya utarejesha uhusiano wake wa kibiashara wa upendeleo na Israel hatua kwa hatua kwa kisingizio cha kutekelezwa usitishaji unaolegalega wa mapigano huko Gaza.
-
Hamas: Israel lazima igharamie ujenzi mpya wa Gaza
Oct 21, 2025 08:01Afisa mwandamizi wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas, Mousa Abu Marzouk ametoa wito kwa Israel kufadhili kikamilifu ukarabati na ujenzi mpya wa Ukanda wa Gaza, akitaja uharibifu mkubwa na haki za Wapalestina zaidi ya milioni mbili ambao wamepoteza makazi yao, makazi na riziki.