-
Amir wa Qatar: Vita vya Israel dhidi ya Ghaza si kingine chochote ila ni mauaji ya kimbari
Oct 21, 2025 03:30Amir wa Qatar Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani amesema, vita vya utawala wa kizayuni wa Israel dhidi ya Ghaza si kitu kingine ila ni mauaji ya kimbari sambamba na kuulaani utawala huo ghasibu kwa kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano.
-
Netanyahu ajigamba kuwa siku ya Jumapili Israel iliidondoshea Ghaza tani 153 za mabomu
Oct 21, 2025 03:30Waziri Mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu amejigamba kuwa jeshi lake lilishambulia Ukanda wa Ghaza siku ya Jumapili kwa tani 153 za mabomu, ambayo ni sawa na kukiri kwamba utawala huo ghasibu umekiuka makubaliano ya kusitisha mapigano uliyofikia na harakati ya Hamas kupitia mpango uliopendekezwa na Rais wa Marekani.
-
Mwakilishi wa US adai vita vya Israel dhidi ya Lebanon haviepukiki ikiwa Hizbullah haitapokonywa silaha
Oct 20, 2025 06:10Tom Barrack, balozi wa Marekani nchini Uturuki na mjumbe maalumu wa masuala ya Syria, ametoa onyo la kutisha kwa Lebanon akiitaka ama iipokonye silaha Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya nchi hiyo Hizbulla au ikabiliwe na mashambulizi mengine ya Israel na migogoro ya kiuchumi na kisiasa.
-
Ripoti: Asilimia 97 ya shule za Gaza zimeharibiwa kwa mashambulizi ya Israel
Oct 19, 2025 23:58Ripoti rasmi zinasema, mashambulizi ya utawala ghasibu wa Israel yameharibu asilimia 97 ya shule za Ukanda wa Gaza na hivyo kuhatarisha mustakbali wa kielimu wa wanafunzi laki tatu wa Kipalestina katika eneo hilo.
-
Iran yailaani Israel kwa kuendelea kuua wanawake na watoto Gaza
Oct 19, 2025 03:10Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baghaei amelaani ukiukaji wa mara kwa mara wa makubaliano ya usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza unaofanywa na utawala ghasibu wa Israel, likiwemo shambulio la hivi karibuni dhidi ya gari lililokuwa limebeba familia ya Kipalestina wakati ikirejea kwenye makazi yao.
-
ICC yatupilia mbali rufaa ya Israel dhidi ya hati za kutiwa nguvuni Netanyahu na Gallant
Oct 18, 2025 23:11Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imekataa ombi la utawala wa kizayuni wa Israel la kukata rufaa dhidi ya hati za kukamatwa waziri mkuu wake Benjamin Netanyahu na aliyekuwa waziri wa vita wa utawala huo ghasibu Yoav Gallant kuhusiana na mauaji ya kimbari yaliyofanywa na jeshi la kizayuni katika Ukanda wa Ghaza.
-
Taa ya kijani ya Trump kwa Israel; Je vita vya Gaza vitaanza tena?
Oct 17, 2025 22:59Rais Donald Trump wa Marekani ameionyesha Israel taa ya kijani ili ianzishe tena vita katika Ukanda wa Gaza.
-
Mkuu wa majeshi ya Yemen auawa katika mashambulizi ya Israel
Oct 17, 2025 03:26Mkuu wa Majeshi ya Yemen, Meja Jenerali Mohammad Abd al-Karim al-Ghamari ameripotiwa kuuawa shahidi katika mashambulizi ya anga ya Israel, pamoja wapamba wake kadhaa na mtoto wake wa kiume aliyekuwa na umri wa miaka 13, Hussein al-Ghamari.
-
Israel yaanza ukhabithi wake, yapunguza misaada ya kuingizwa Ghaza hadi nusu, yazuia fueli kikamilifu
Oct 15, 2025 02:33Utawala wa kizayuni wa Israel umeueleza Umoja wa Mataifa kwamba, kuanzia leo Jumatano utaruhusu malori 300 tu ya misaada kwa siku, ikiwa ni nusu ya idadi iliyokubaliwa kuingia katika Ukanda wa Ghaza na kwamba hakuna mafuta yoyote au gesi itakayoruhusiwa kuingizwa katika eneo hilo isipokuwa kwa mahitaji maalumu yanayohusiana na miundombinu ya kibinadamu.
-
Afrika Kusini: Kesi ya mauaji ya kimbari tuliyofungua ICJ dhidi ya Israel itaendelea licha ya vita kusitishwa
Oct 15, 2025 02:32Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amesema usitishaji vita wa Ghaza hautaathiri kesi ya mauaji ya kimbari iliyofunguliwa na nchi yake dhidi ya utawala wa kizayuni wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ).