-
Kwa nini Tume ya Ulaya haikubali hata maneno ya mwakilishi wake yenyewe kuhusu mauaji ya kimbari huko Gaza?
Sep 07, 2025 23:01Siku ya Ijumaa, Agosti 5, Kamisheni ya Umoja wa Ulaya ilipuuza kauli ya Teresa Ribera, Naibu MKuu Mtendaji wake kuhusu mauaji ya kimbari ya Israel katika Ukanda wa Gaza, na kudai kwamba jinai hizo zinaweza tu kuthibitishwa na mahakama husika.
-
Saudia yalitaka Baraza la Usalama lisitishe 'sera za uchokozi' za Israel huko Gaza
Sep 06, 2025 08:05Saudi Arabia imelaani mipango ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu ya kuwafurusha kwa nguvu Wapalestina kutoka Gaza, ikilitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuingilia kati na kukomesha "sera za uchokozi" za Tel Aviv dhidi ya wananchi wa Palestina na ardhi yao.
-
Mediapart: 2024 Israel iliweka 'rekodi ya mwaka' ya ununuzi wa silaha kutoka Ufaransa
Sep 06, 2025 02:48Uuzaji wa silaha wa Ufaransa kwa utawala wa kizayuni wa Israel katika mwaka uliopita wa 2024 ulifikia kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa katika kipindi cha miaka minane iliyopita sambamba na kuwepo ongezeko kubwa la mauzo ya silaha za Ufaransa duniani kote. Hayo ni kwa mujibu wa gazeti la ripoti za uchunguzi nchini humo la Mediapart.
-
Jeshi la kizayuni laporomosha jengo la ghorofa 12 linalowapa hifadhi mamia ya Wapalestina Ghaza
Sep 05, 2025 23:36Jeshi la utawala wa kizayuni wa Israel siku ya Ijumaa liliripua na kuporomosha jengo la ghorofa 12 la makazi ya raia magharibi mwa Mji wa Ghaza linalowapa hifadhi mamia ya Wapalestina waliolazimika kuyahama makazi yao katika eneo hilo lenye msongamano wa watu na ambalo limekuwa kimbilio la makumi ya maelfu ya Wapalestina.
-
Kiongozi wa Wadruze Syria amshukuru Trump, Israel na EU, asisitizia msimamo wa jamii yao kujitawala
Sep 05, 2025 23:35Kiongozi wa kiroho wa jamii ya Wadruze wa Syria, Hikmat al-Hijri ametoa shukurani kwa Marekani, utawala wa kizayuni wa Israel na nchi za Ulaya, akisisitiza kwamba haki ya kujiamualia mustakabali wao ni haki takatifu inayodhaminiwa na mikataba yote ya kimataifa.
-
Bunge la Scotland lapiga kura ya kuisusia, kuiwekea vikwazo Israel kwa mauaji ya kimbari Gaza
Sep 05, 2025 07:06Bunge la Scotland limepiga kura ya kutaka kusisiwa mara moja Israel na kampuni za utawala huo wa Kizayuni zinazotuhumiwa kuhusika na mauaji ya kimbari huko Gaza.
-
Watu wa Afrika walaani jinai za utawala wa Israel dhidi ya Yemen na Gaza
Sep 05, 2025 06:54Wananchi wa nchi kadhaa za Afrika wamefanya maandamano makubwa kulaani jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wa Yemen na Gaza, wakionesha mshikamano wa wazi na harakati za ukombozi wa Wapalestina.
-
Kwa nini mgawanyiko kati ya bunge la Uingereza na serikali kuhusu mgogoro wa Gaza unaendelea?
Sep 03, 2025 23:03Wabunge wa Uingereza sanjari na kukosoa sera za serikali ya Waziri Mkuu Keir Starmer katika vita vya Gaza wameishutumu serikali ya London kwa kuilegezea Israel.
-
Spika wa Iran: Waislamu wana wajibu wa kukomesha mauaji ya Israel Gaza
Sep 03, 2025 03:43Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) ameyataka mataifa ya Kiislamu kuungana katika vita dhidi ya utawala wa Kizayuni, ambao ameutaja kuwa shetani mkubwa zaidi duniani.
-
Kamanda Mousavi: Jeshi la Iran liko tayari kutoa jibu chungu kwa uchokozi wowote
Sep 03, 2025 03:08Mkuu wa Majeshi ya Iran, Meja Jenerali Abdolrahim Mousavi amesisitiza kuwa vikosi vya ulinzi vya taifa hili viko imara na tayari kutoa jibu madhubuti na chungu kwa uchokozi wowote mpya wa maadui.