-
Ansarullah: Operesheni za kushambulia meli zenye uhusiano na Israel zitapanuliwa hadi Bahari ya Hindi
Mar 15, 2024 04:11Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen, Sayyid Abdul Malik Al-Houthi amesema askari wa jeshi la nchi hiyo wataendelea na operesheni zao za kujibu mapigo dhidi ya meli za kibiashara zenye uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel, kwa kuzizuia meli hizo kupita hata kwenye eneo la maji ya Bahari ya Hindi na Rasi ya Tumaini Jema.
-
Naledi Pandor: Raia wa Afrika wanaoshiriki katika vita dhidi ya Gaza wakirejea watakamatwa
Mar 14, 2024 11:24Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Afrika Kusini amesema kuwa, raia yeyote wa nchi hiyo atakayeusaidia utawala wa Kizayuni katika vita vya Ukanda wa Gaza atatiwa mbaroni punde tu atakaporejea Afrika Kusini.
-
HAMAS yakanusha madai ya kukubali pendekezo la usitishaji vita
Mar 13, 2024 04:15Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imekadhibisha ripoti ya shirika la habari la al-Arabiya kwamba kundi hilo la muqawama limeafiki 'pendekezo la kimataifa' la usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza.
-
Waisraeli 80,000 wakimbia makazi yao wakihofia makombora ya Hizbullah
Mar 13, 2024 04:14Makumi ya maelfu ya walowezi wa Kizayuni wamekimbia makazi yao katika maeneo ya kaskazini mwa Palestina yaliyopachikwa jinai bandia la Israel, wakihofia mashambulizi ya Harakati ya Hizbullah ya Lebanon.
-
Mamia ya walowezi wa Kiyahudi wauvamia Msikiti wa Al-Aqsa huku wakilindwa na askari wa Israel
Mar 12, 2024 23:17Mamia ya walowezi wa Kiyahudi jana Jumanne walivamia tena eneo la Msikiti wa Al-Aqsa katika mji wa Baitul-Muqaddas Mashariki unaokaliwa kwa mabavu huku wakisindikizwa na kulindwa na wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wanaoendelea kuchukua hatua kali za kuwawekea mipaka Wapalestina ya kuingia kwenye msikiti huo.
-
Intelijensia ya Marekani: HAMAS itaendelea kutoa changamoto kwa Israel kwa "miaka kadhaa"
Mar 12, 2024 23:16Ripoti ya tathmini ya kiintelijensia iliyotolewa na Marekani imetilia shaka uwezo wa utawala wa Kizayuni wa Israel wa kuifuta Hamas, harakati hiyo ya muqawama ya Palestina huenda ikatoa changamoto "ya muda mrefu" kwa miaka kadhaa kwa utawala huo ghasibu unaokalia ardhi za Palestina kwa mabavu.
-
Syria: Kuunga mkono jinai za Netanyahu kumefichua dhati ya Wamagharibi
Mar 11, 2024 07:53Waziri wa Mambo ya Nje wa Syria amezikosoa vikali nchi za Magharibi kwa kuendelea kuunga mkono jinai za kivita zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza na kusisitiza kuwa, uungaji mkono huo umefichua dhati halisi ya Wamagharibi.
-
Wapalestina watano wauawa na misaada wa kudondoshwa kutoka angani, Gaza
Mar 09, 2024 08:19Wapalestina watano wameuawa na vifurushi vya misaada vilivyodondoshwa na ndege za Marekani na washirika wake kwenye Ukanda wa Gaza unaozingirwa na Israel, huku mamlaka ya Gaza ikilishutumu zoezi hilo kuwa ni "propaganda tupu" na sio huduma ya kibinadamu.
-
Iran yaiambia UN: Tuna haki halali ya kujibu vitisho vya Israel
Mar 08, 2024 04:38Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema Jamhuri ya Kiislamu ina kila haki na uhalali wa kuchukua hatua zote inazoweza kujibu uchokozi na tishio lolote kutoka utawala wa Israel dhidi ya usalama wake wa taifa na maslahi ya nchi hii.
-
HAMAS: Israel imetibua juhudi zote za kusitisha vita Gaza
Mar 08, 2024 03:53Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imesema utawala haramu wa Israel umevuruga jitihada zote za wapatanishi za kufikiwa makubaliano ya usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza.