-
Marekani yafanya kimya kimya mauzo 100 ya silaha kwa Israel
Mar 08, 2024 00:10Ripoti mpya imefichua kuwa, Marekani imeidhinisha kimya kimya mauzo 100 ya silaha kwa Israel tangu utawala huo wa Kizayuni uanzishe vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza Oktoba 7, 2023.
-
Vyombo vya habari vya Uingereza vinawaonyesha Waisraeli waathiriwa zaidi kuliko Wapalestina
Mar 07, 2024 08:43Imebainika kuwa "upendeleo mkubwa" unafanywa na vyombo vya habari vya Uingereza katika utangazaji wa matukio ya Ukanda wa Ghaza tangu Oktoba 7, kutokana na kutumia "lugha ya hisia" inayowaonyesha Waisraeli kuwa ni wahanga na waathiriwa wa mashambulizi mara 11 zaidi kulinganisha na Wapalestina.
-
Chuki dhidi ya Waislamu zimeongezeka Japan tangu Israel ilipoanza kuishambulia kijeshi Ghaza
Mar 07, 2024 08:30Mwanaakademia wa Kijapan, Kayyim Naoki Yamamoto amesema, hisia za chuki dhidi ya Waislamu nchini Japan zinaongezeka tangu utawala haramu wa Kizayuni wa Israel ulipoanzisha vita vya kikatili na mashambulio ya kinyama dhidi ya Ukanda wa Ghaza Oktoba 7, 2023.
-
Ukosoaji wa UN wa mashambulizi ya makusudi ya Israel dhidi ya misafara ya misaada huko Gaza
Mar 06, 2024 08:01Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Haki ya Chakula ametangaza kwamba, jeshi la Israel linashambulia kwa makusudi misafara ya misaada ya kibinadamu huko Gaza licha ya kujua njia za misafara hiyo.
-
Kuongezeka uungaji mkono wa wananchi wa Marekani kwa Wapalestina
Mar 05, 2024 04:12Matokeo ya uchunguzi wa maaoni uliofanywa na jarida la Wall Street Journal yanaonyesha kuwa, wananchi wengi wa Marekani hawaridhishwi na utendaji kazi wa Rais Joe Biden katika vita vya Gaza.
-
Iran: OIC inakabiliwa na 'mtihani mgumu' kuhusu uhalifu wa Israel, himaya ya Marekani kwa utawala huo
Mar 05, 2024 04:11Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesisitiza umuhimu wa mkutano wa dharura wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) unaotarajiwa kufanyika leo, akisema jumuiya hiyo yenye wanachama 57 "inakabiliwa na mtihani" juu ya vita vya mauaji ya kimbari vya Israel kwenye Ukanda wa Gaza.
-
Mamia waandamana nje ya ubalozi wa Israel, Washington kulaani vita Gaza
Mar 03, 2024 04:10Mamia ya watu wamefanya maandamano mbele ya ubalozi wa Israel mjini Washington, Marekani kulaani vita vya mauaji ya kimbari vinavyoendelezwa na utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza.
-
EU yaikosoa Israel kwa kuzuia misaada ya kibinadamu Gaza
Mar 03, 2024 04:09Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amekosoa hatua ya utawala haramu wa Israel ya kuzuia kuingizwa na kusambazwa misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Gaza.
-
Wanajihadi wa HAMAS wadhibiti ndege isiyo na rubani ya Israel
Mar 03, 2024 04:09Wanamapambano wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS wametangaza habari ya kutwaa na kudhibiti ndege isiyo na rubani ya Israel (droni), ikiwa ni kuendelea kujibu jinai za Wazayuni dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Israel yapuuza malalamiko ya dunia, yaendelea kumwaga damu za Wapalestina
Mar 02, 2024 08:19Kwa akali Wapalestina 17 wameuawa shahidi katika mashambulizi mapya ya anga ya utawala wa Kizayuni wa Israel yaliyolenga nyumba tatu za Wapalestina katika maeneo ya Deir el-Balah na Jabalia katika Ukanda wa Gaza.