-
Baada ya mazungumzo ya Moscow, mirengo ya Palestina yaapa kuungana pamoja dhidi ya Israel
Mar 01, 2024 23:37Makundi ya Palestina ikiwemo Hamas na Fat-h yamesema yatafuata "umoja wa kivitendo" katika kukabiliana na utawala wa Kizayuni wa Israel baada ya wawakilishi wao kukutana katika mazungumzo yaliyoandaliwa na Russia mjini Moscow.
-
Ben-Gvir awapongeza wanajeshi wa Israel walioua zaidi ya Wapalestina 100 Ghaza, US yaizuia UN isitoe tamko
Mar 01, 2024 23:37Waziri wa utawala haramu wa Kizayuni wa Israel mwenye misimamo mikali ya chuki amewapongeza wanajeshi wa utawala huo walioua zaidi ya Wapalestina 100 waliokuwa wakisubiri misaada ya kibinadamu katika Ukanda wa Ghaza uliowekewa mzingiro.
-
Haniyeh awataka Wapalestina kuandamana kwenye Msikiti wa Al-Aqsa siku ya 1 ya Ramadhani
Feb 29, 2024 08:37Mkuu wa Ofisi ya Siasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) amewataka Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu na Israel kuandamana hadi Msikiti wa Al-Aqsa katika siku ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.
-
Waingereza waitaka London iache kuipa silaha Israel
Feb 28, 2024 03:18Wanaharakati wa haki nchini Uingereza wamefanya maandamano makubwa ya kuitaka serikali ya nchi hiyo isitishe mauzo ya silaha kwa utawala haramu wa Israel.
-
Maduro akosoa jinai za kikoloni za Israel dhidi ya Palestina
Feb 28, 2024 03:16Rais Nicolas Maduro wa Venezuela amesema jinai na mashambulizi ya kinyama yanayofanywa na Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza ni ishara ya wazi kuwa utawala wa Kizayuni unaendeleza malengo ya kikoloni dhidi ya Palestina.
-
Maandamano yafanyika Washington na Los Angeles US kumuenzi askari aliyejichoma moto kulalamikia jinai za Israel
Feb 28, 2024 00:16Wamarekani wameandamana katika miji ya Washington na Los Angeles kumuenzi mwanajeshi wa nchi hiiyo aliyejichoma moto kuwaunga mkono wananchi wa Palestina na kulalamikia jinai za kinyama za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi hao madhulumu.
-
OIC yaziomba nchi zote duniani zisiuuzie silaha utawala wa Kizayuni wa Israel
Feb 27, 2024 07:50Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) amezitaka nchi zote duniani kuacha kutuma silaha na zana za kijeshi kwa utawala unaofanya mauaji ya kimbari wa Israel.
-
Ngome za Israel zanyeshewa kwa 'mvua' ya makombora ya Hizbullah
Feb 25, 2024 06:25Wanajihadi wa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebaon wameshambulia kwa makombora na maroketi kambi kadhaa za utawala wa Kizayuni katika ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu usiku wa kuamkia leo.
-
Wataalamu wa UN: Kuipelekea silaha Israel kukomeshwe mara moja!
Feb 24, 2024 23:05Kundi la wataalamu wa Umoja wa Mataifa limeonya kwamba upelekaji wowote wa silaha au risasi kwa utawala wa Kizayuni wa Israel ambazo zitatumika katika mashambulizi ya ardhini na angani dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghazza uliozingirwa unaweza ukawa unakiuka sheria za kimataifa za kibinadamu, na lazima ukomeshwe mara moja.
-
Idhini mpya ya Uingereza kwa Israel ya kuendeleza mauaji ya umati dhidi ya wananchi wa Palestina
Feb 23, 2024 04:57Uingereza ambayo ni moja ya waungaji mkono wakuu wa jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina sambamba na Ujerumani na Marekani, hivi sasa imetoa idhini mpya kwa Israel ya kuendeleza mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina hasa wa Ghazza. Madola hayo matatu ya Magharibi ndiyo yaliyoko mstari wa mbele katika kuusheheneza silaha hatari utawala wa Kizayuni ili uzidi kuua raia wa Palestina hasa wanawake na watoto wadogo.