-
Sisitizo la Mawaziri wa Mambo ya Nje wa EU juu ya kulinda makubaliano ya JCPOA na kuimarisha usalama wa Ghuba ya Uajemi
Aug 31, 2019 07:40Umoja wa Ulaya pamoja na Troika ya Ulaya zikiwa wanachama wa kundi la 4+1 mara kadhaa zimesisitiza kuwa kuna udharura wa kuyalinda makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na wakati huo huo kurejesha uthabiti na usalama katika Ghuba ya Uajemi kwa kuzingatia chokochoko za Marekani katika eneo hilo la maji lenye umuhimu wa kijio-stratejia.
-
Zarif: Lazima Marekani isitishe ugaidi wa kiuchumi na irejee JCPOA, kabla ya mazungumzo
Aug 30, 2019 03:30Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Mohammad Javad Zarif amesema Marekani lazime irejee katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA na isitishe ugaidi wake wa kiuchumi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kabla ya kufanyika mazungumzo.
-
Kudumu kwa JCPOA kunategemea hatua za kivitendo za Ulaya, si kufanya mazungumzo na Marekani
Aug 29, 2019 07:43Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anayehusika na masuala ya kisiasa amesema, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitaruhusu Marekani iyatumie vibaya kwa manufaa yake mazungumzo ya Iran na nchi za Ulaya.
-
Safari ambayo haikutarajiwa ya Zarif nchini Ufaransa; muendelezo wa mazungumzo, mara hii Bairritz
Aug 26, 2019 08:58Mohammad Javad Zarif, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Jumapili alasiri alielekea Ufaransa katika safari ambayo haikuwa imetaraijiwa kufuatia mwaliko wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa Jean-Yves Le Drian kwa lengo la kuendelea na mazungumzo kuhusu ubunifu wa hivi karibuni wa marais wa Iran na Ufaransa kuhusu mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Ukosoaji wa Mkuu wa Baraza Ulaya dhidi ya siasa za kuzusha mizozo za Rais Donald Trump
Aug 26, 2019 03:45Siasa na hatua za Rais Donald Trump wa Marekani katika nyanja mbalimbali hususan kuiondoa Washington katika mikataba na makubaliano ya kimataifa kama ya nyuklia ya JCPOA, mkataba wa mabadiliko ya tabianchi wa Paris Ufaransa na vilevile hatua yake ya kung'ang'ania kuwa na vita vya kibiashara na madola mengine makubwa kiuchumi duniani, ni mambo ambayo yamepelekea kuibuka mizozo mikubwa katika uga wa kimataifa.
-
Mazungumzo ya viongozi wa Ufaransa na Marekani kuhusu Iran na JCPOA
Aug 25, 2019 08:21Mivutano iliyopo baina ya Marekani na nchi za Ulaya zilizomo katika kundi la 4+1 kuhusiana na jinsi ya kuamiliana na Iran na kadhia nzima ya mapatano ya nyuklia ya JCPOA bado ni moja ya mivutano mikubwa ya pande hizo mbili. Katika wiki za hivi karibuni, Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa alifanya mazungumzo mbalimbali na marais wa Iran na Marekani na kuja na mapendekezo ya kupunguza wasiwasi uliopo.
-
Dakta Zarif: Madola ya Ulaya yatekeleze kivitendo ahadi zao za JCPOA
Aug 24, 2019 07:53Waziri wa Mashauri yay Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, endapo madola ya Ulaya yatatekeleza kivitendo ahadi zao za makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, basi Iran nayo iko tayari kuachana na hatua ilizochukua za kupunguza uwajibikaji wake kwa mujibu wa makubaliano hayo.
-
Sisitizo la Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Russia na Ujerumani juu ya kulindwa makubaliano ya nyuklia ya JCPOA
Aug 23, 2019 02:50Baada ya Marekani kujiondoa kinyamela katika makubaliano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) Mei mwaka jana, kinyume na matarajio ya Washington ambayo ilitaka nchi zingine wanachama wa kundi la 5+1 nazo zichukue uamuzi kama wake, mataifa hayo ikiwemo Russia na Ujerumani yalisisitiza juu ya kuendelea kubakishwa makubaliano hayo ya kimataifa yaliyokuwa yamepata baraka kamili za Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Rouhani: Kujiondoa Marekani katika JCPOA kuna maana ya kukiuka makubaliano ya kimataifa na ugaidi wa kiuchumi
Aug 22, 2019 22:15Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kujiondoa Marekani katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA kuna maana ya kuvunja mkataba, kukiuka ahadi, kupuuza makubaliano ya kimataifa na ugaidi wa kiuchumi.
-
Zarif: Nchi za Ulaya bado hazijatekeleza ahadi zao katika mapatano ya JCPOA
Aug 21, 2019 20:42Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameashiria kufungamna Iran na mapatano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezwaji (JCPOA) na kusema: "Baada ya Mareakni kujiondoa katika mapatano haya, nchi za Ulaya hazijatekeleza ahadi zao."