-
Rais Rouhani: Hatua zilizochukuliwa hadi sasa ni chanya kwa ajili ya kuendeleza JCPOA
May 27, 2018 03:12Rais Hassan Rouhani amesema, baada ya Marekani kujitoa kwenye makubaliano ya JCPOA waliowengi katika jamii ya kimataifa wameipa haki Iran na kuyatetea makubaliano hayo na kuongeza kwamba hatua zilizochukuliwa hadi sasa ni nzuri kwa ajili ya kuendeleza makubaliano hayo ya nyuklia.
-
Zarif: Iran haijafanya mazungumzo na Ulaya kuhusu uwezo wake wa makombora na ushawishi kieneo
May 26, 2018 10:57Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekanusha kuwepo mazungumzo na nchi za Ulaya kuhusu uwezo wa makombora ya Tehran wala kuhusu ushawishi wake katika eneo.
-
Russia: Baada ya kujiondoa JCPOA, Marekani haina haki yoyote kuhusiana na makubaliano hayo
May 26, 2018 02:47Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imesisitiza kwamba kitendo cha Marekani kujiondoa katika makubaliano ya nyuklia ya Iran maarufu kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA), kimeiondolea nchi hiyo haki yoyote kuhusiana na makubaliano hayo.
-
Sisitizo la Putin na Macron la kulindwa mapatano ya JCPOA
May 25, 2018 09:04Akizungumza mara tu baada ya kuonana na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa, Rais Vladimir Putin wa Russia amesisitiza juu ya umuhimu wa kulindwa mapatano ya nyuklia kati ya Iran na nchi kubwa za dunia, mashuhuri kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) na kuusifu msimamo wa Ufaransa na nchi nyingine za Ulaya kuhusiana na kudumishwa utekelezaji wa mapatano hayo.
-
Mogherini: Kuyadumisha makubaliano ya JCPOA ni mtihani kwa Umoja wa Ulaya
May 24, 2018 22:49Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya amesema kuyalinda na kuyadumisha makubaliano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji (JCPOA) ni mtihani kwa Umoja wa Ulaya.
-
Kiongozi Muadhamu: Ikiwa Ulaya itazembea, lran ina haki ya kuanzisha shughuli zake za nyuklia
May 24, 2018 00:21Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria uadui wa msingi, wa kina na endelevu wa Marekani dhidi ya mfumo wa Kiislamu na taifa la Iran na kusisitiza kwamba bila shaka Iran itaishinda tu Marekani iwapo viongozi wa Iran watatekeleza vilivyo majukumu yao.
-
Radiamali ya Ulaya kuhusiana na stratijia mpya ya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
May 23, 2018 23:38Federica Mogherini, Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya ametoa radiamali yake kupitia tovuti rasmi ya umoja huo kufuatia stratijia mpya iliyotangazwa na Mike Pompeo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani dhidi ya Iran, akitangaza kufungamana kikimilifu EU na makubaliano ya nyuklia ya Iran maaruku kwa jina la JCPOA.
-
Matamshi yaliyo dhidi ya Iran ya Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani
May 21, 2018 23:35Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani amekariri madai yaliyo dhidi ya Iran na kwa mara nyingine tena kuituhumu Tehran kuwa inasababisha ukosefu wa amani katika eneo.
-
Qassemi: Nchi za Ulaya zitoe dhamana kuwa maslahi ya Iran yatazingatiwa katika mapatano ya JCPOA
May 21, 2018 08:47Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema: "Katika muda mfupi uliosalia, nchi za Ulaya zinapaswa kutoa dhamana kuwa maslahi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yatalindwa baada ya Marekani kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA."
-
Iran haitafanya mazungumzo kuhusu maudhui yoyote isipokuwa Mapatano ya Nyuklia ya JCPOA
May 21, 2018 07:51Karibu wiki mbili baada ya Marekani kujiondoa katika mapatano ya nyuklia ya Iran yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekeelzwaji, JCPOA, kumefanyika mazungumzo mjini Brussels baina ya wakuu wa Iran na Umoja wa Ulaya.