-
Gavana wa Nairobi apandishwa kizimbani, akana mashtaka yanayomkabili
Dec 09, 2019 08:54Gavana wa jiji la Nairobi nchini Kenya Mike Mbuvi Sonko, amekana mashtaka yanayomkabili, ya ufisadi na uhalifu wa kiuchumi unaohusisha mamilioni ya dola, wakati alipofikishwa mahakamani mapema leo.
-
Shambulizi la al-Shabaab dhidi ya basi la abiria laua 10 Kenya
Dec 07, 2019 03:45Watu 10 wamethibitishwa kuuawa katika shambulizi dhidi ya basi la abiria linaloaminika kufanywa na genge la kigaidi na kitakfiri al-Shabaab katika kaunti ya Wajir, kaskazini mashariki mwa Kenya mpakani na Somalia.
-
Viongozi wa Kenya wazindua ripoti ya BBI + Sauti
Nov 28, 2019 03:32Viongozi nchini Kenya wamezindua ripoti ya uwiano na utangamano wa kisiasa huku wakifanya juhudi za kuleta muamko mpya wa kisiasa na mshikamano katika kila fani ya maisha nchini humo. Seifullah Murtadha na maelezo zaidi kutoka Mombasa...
-
Zaidi ya familia 50 zahamishwa katika mpaka wa Uganda na Kenya kutokana na mafuriko + Sauti
Nov 25, 2019 12:10Familia zaidi ya 50 zimehamishwa kutoka kwenye mpaka wa Uganda na Kenya kutokana na kuhofia maafa yanayoweza kusababishwa na mvua kubwa zinazonyesha mfululizo. Kigozi Ismail na ripoti zaidi kutoka Kampala.
-
SAUTI, Mkasa wa kusikitisha kuhusiana na tukio la maporomoko ya ardhi na mafuriko nchini Kenya
Nov 25, 2019 07:40Viongozi wa serikali ya Kenya wametangaza habari ya kuongezeka idadi ya wahanga wa mafuriko na maporomoko ya ardhi kuwa imefikia watu 60.
-
Watu 24 wapoteza maisha katika maporomoko ya ardhi Kenya
Nov 23, 2019 09:44Watu wasiopungua 24 wamepoteza maisha magharibi mwa Kenya kufuatia maporomoko ya ardhi katika Kaunti ya West Pokot.
-
UNFPA yataka dhuluma dhidi ya wanawake katika jamii zikomeshwe
Nov 14, 2019 10:58Mmoja kati ya wanawake watatu duniani hukumbana na dhuluma za kijinsia kutoka kwa wapenzi au waume zao.
-
Rais Kenyatta afuta ajenda ya ubaradhuli katika Kongamano la Kimataifa Nairobi
Nov 10, 2019 03:57Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amefutilia mbali mpango wowote wa kujumuishwa kadhia ya ubaradhuli kama moja ya ajenda za Kongamano la Kimataifa la Idadi ya Watu litakalofanyika wiki ijayo katika mji mkuu wa nchi hiyo, Nairobi.
-
Wakenya laki moja waishtaki Uingereza kutokana na jinai za ukoloni wake
Oct 30, 2019 10:31Zaidi ya Wakenya 100,000 wamewasilisha mashtaka kwa Umoja wa Mataifa dhidi ya utawala wa kikoloni wa Uingereza kutokana na jinai ya kuwapora ardhi zao zenye rutuba na kuwapeleka sehemu kame.
-
SAUTI, Serikali ya Kenya: Hadi sasa watu 29 wamepoteza maisha kutokana na mafuriko ya mvua zinazonyesha nchini
Oct 24, 2019 13:24Serikali ya Kenya imethibitisha kufariki dunia watu 29 kutokana na mafuriko yanayotokana na mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo tofauti ya nchi hiyo.