-
Trump atishia vikwazo vikali zaidi baada ya Korea Kaskazini kufanyia majaribio kombora jipya
May 14, 2017 07:51Rais Donald Trump wa Marekani ametishia kuiwekea vikwazo vikali zaidi Korea Kaskazini, baada ya Pyongyang kufyatua kifaa kinachoaminika kuwa kombora lake la balestiki kuelekea upande wa Japan.
-
Jaribio la Kutaka Kumuua Kiongozi wa Korea Kaskazini ni tangazo la vita
May 12, 2017 07:20Korea Kaskazini imelaani tena jaribio la kutaka kumuua kiongozi wake ambalo limetekelezwa na mashirika ya kijasusi ya Marekani na Korea Kusini na kulitaja jaribio hilo kuwa sawa na tangazo la vita.
-
Rais wa Korea Kusini yupo tayari kuitembelea nchi jirani ya Korea Kaskazini
May 11, 2017 03:31Rais mpya wa Korea Kusini Moon Jae-in amefungua urais wake kwa kutangaza kuwa yuko tayari kuitembelea Korea Kaskazini iwapo mazingira yataruhu ikiwa ni katika kutekeleza ahadi za uchaguzi za kufanya mazungumzo na nchi hiyo hasimu.
-
China yaipa sharti Marekani kumuuzulu kamanda wake, mkabala na kuishinikiza Pyongyang
May 08, 2017 15:11China imempa sharti Rais Donald Trump wa Marekani la kumuuzulu kamanda wa vikosi vya nchi hiyo vilivyoko Korea Kusini mkabala na Beijing kuishinikiza Korea Kaskazini.
-
Korea Kaskazini yawataka raia wa Korea Kusini kususia uchaguzi ujao wa rais
May 08, 2017 04:05Gazeti la serikali ya Korea Kaskazini la Rodong Sinmun limewataka raia wa nchi jirani ya Korea Kusini kususia uchaguzi ujao wa rais wa nchi hiyo kwa lengo la kuwaondoa madarakani watawala wenye mahusiano na Marekani.
-
Korea Kaskazini: CIA inapanga kumuua kiongozi wetu kwa silaha za kemikali
May 06, 2017 04:15Pyongyang imesema Shirika la Ujasusi la Marekani (CIA) linapanga njama ya kumuua kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un kwa kushirikiana na Idara ya Intelijensia ya Korea Kusini.
-
China yaijibu Korea Kaskazini baada ya malalamiko ya Pyongyang dhidi yake
May 05, 2017 07:14China imetoa jibu na radiamali kwa ripoti kali iliyotolewa na Shirika rasmi la Habari la Korea Kaskazini dhidi yake na kueleza kuwa siasa zake kuhusiana na Pyongyang daima zimekuwa za insafu na usawa na zisizo za nia mbaya.
-
Onyo la Korea Kaskazini kwa China kuhusiana na silaha za nyuklia na makombora ya Pyongyang
May 05, 2017 07:13Alkhamisi ya jana serikali ya Korea Kaskazini, sambamba na kukosoa vikali siasa za Uchina kuhusiana na shughuli za nyuklia na makombora yake, ilisema kuwa, kuwa na mahusiano ya kirafiki na nchi hiyo jirani haihitaji kuipigia magoti Beijing.
-
Onyo la Korea Kaskazini kwa Marekani juu ya uwezekano wa kutokea vita vya nyuklia baina yao
May 03, 2017 07:36Hatua ya Marekani ya kurusha ndege zake zenye uwezo mkubwa wa kushambulia kwa mabomu aina ya Supersonic B-1B Lancer kwenye anga ya Peninsula ya Korea, imeibua radiamali kali kutoka kwa Korea Kaskazini na kuifanya nchi hiyo kutangaza kuwa, hatua ya kujionyesha na utumiaji mabavu ya Washington katika eneo hilo, inakaribisha kutokea kwa vita ya nyuklia.
-
Korea Kaskazini: Ikiwa meli za US zitatukaribia, tutazigeuza kuwa vyuma chakavu
May 01, 2017 14:14Kwa mara nyingine serikali ya Korea Kaskazini imeitahadharisha Marekani kwamba, ikiwa meli za kivita za nchi hiyo zitaendelea kuwepo katika Peninsula ya Korea, basi itaziangamiza silaha za nyuklia za Washington na kuzigeuka kuwa vyuma chakavu.