-
Onyo la Korea Kaskazini kwa China kuhusiana na silaha za nyuklia na makombora ya Pyongyang
May 05, 2017 02:43Alkhamisi ya jana serikali ya Korea Kaskazini, sambamba na kukosoa vikali siasa za Uchina kuhusiana na shughuli za nyuklia na makombora yake, ilisema kuwa, kuwa na mahusiano ya kirafiki na nchi hiyo jirani haihitaji kuipigia magoti Beijing.
-
Onyo la Korea Kaskazini kwa Marekani juu ya uwezekano wa kutokea vita vya nyuklia baina yao
May 03, 2017 03:06Hatua ya Marekani ya kurusha ndege zake zenye uwezo mkubwa wa kushambulia kwa mabomu aina ya Supersonic B-1B Lancer kwenye anga ya Peninsula ya Korea, imeibua radiamali kali kutoka kwa Korea Kaskazini na kuifanya nchi hiyo kutangaza kuwa, hatua ya kujionyesha na utumiaji mabavu ya Washington katika eneo hilo, inakaribisha kutokea kwa vita ya nyuklia.
-
Korea Kaskazini: Ikiwa meli za US zitatukaribia, tutazigeuza kuwa vyuma chakavu
May 01, 2017 09:44Kwa mara nyingine serikali ya Korea Kaskazini imeitahadharisha Marekani kwamba, ikiwa meli za kivita za nchi hiyo zitaendelea kuwepo katika Peninsula ya Korea, basi itaziangamiza silaha za nyuklia za Washington na kuzigeuka kuwa vyuma chakavu.
-
HAMAS yaishukuru Korea Kaskazini, Wazayuni walaumiana kwa kuichokoza Pyongyang
May 01, 2017 03:02Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa tamko na kuipongeza Korea Kaskazini kwa msimamo wake thabiti dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Korea Kaskazini yasema itaiadhibu vikali Israel
Apr 30, 2017 02:51Korea Kaskazini imesema itauadhibu vikali utawala haramu wa Israel kwa kuthubutu kuuvunjia heshima uongozi wa nchi hiyo.
-
Korea Kusini: Tupo tayari kuzungumza na Korea Kaskazini kutatua tofauti
Apr 27, 2017 11:27Serikali ya Korea Kusini imetangaza azma yake ya kufanya mazungumzo na Korea Kaskazini kwa ajili ya kutatua tofauti zilizopo baina yao.
-
Kupamba moto tena mikwaruzano kati ya Korea Kaskazini na Marekani
Apr 25, 2017 22:02Sambamba na kuwadia maadhimisho ya mwaka wa 85 wa kuasisiwa jeshi la Korea Kaskazini na kukaribia kutimia siku 100 tangu Donald Trump atawazwe kuwa rais wa Marekani mikwaruzano ya kisiasa baina ya Pyongyang na Washington imeshtadi na kuzidi kupamba moto.
-
Korea Kaskazini: Marekani ima ijisalimishe kwa njia ya kisiasa au ichague vita
Apr 25, 2017 10:31Katika sherehe za mwaka wa 85 wa kuundwa jeshi la Korea Kaskazini serikali ya Pyongyang imetoa onyo kali kwa Marekani na kuikumbusha kuwa, inatakiwa ichague moja ya njia mbili, ima ijisalimishe kisiasa au ichague njia ya kijeshi.
-
Korea Kaskazini imewatia nguvuni raia 3 wa Marekani
Apr 23, 2017 22:56Katika hali ambayo taharuki ingali imetanda katika Peninsula ya Korea, serikali ya Korea Kaskazini imemtia mbaroni raia wa Marekani, na kupelekea idadi ya Wamarekani wanaozuiliwa na serikali ya Pyongyang hadi sasa kufikia watatu.
-
Indhari ya Korea Kaskazini kwa China kuhusiana na vikwazo vya kiuchumi dhidi yake
Apr 23, 2017 08:13Serikali ya Korea Kaskazini imeionya China kwamba, ikiwa itaendeleza vikwazo vya kiuchumi dhidi yake, basi uhusiano wa nchi hizo mbili utapata madhara makubwa.