Aug 28, 2020 10:12
Takriban ni miongo 7 sasa ambapo Marekani ina wanajeshi wake katika Rasi ya Korea. Licha ya kufanyika mazungumzo mara kadhaa baina ya viongozi wa Marekani na Korea Kaskazini kuhusu kupokonywa silaha za nyuklia Pyongyang lakini mgogoro wa Korea mbili bado uko vile vile. Si hayo tu lakini rais wa Marekani, Donald Trump hivi sasa anataka kupunguzwa idadi ya wanajeshi wa nchi hiyo huko Korea Kusini, suala ambalo limezusha mzozo mpya.