-
Serikali ya Libya yapinga ombi la Haftar la kusimamishwa vita bila ya kuondoka wanamgambo wake
Dec 06, 2019 07:30Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Libya imekataa ombi la jenerali muasi Khalifa Haftar la kusimamishwa vita bila ya wapiganaji wa jenerali huyo kuondoka katika maeneo waliyoyateka. Kundi linaloongozwa na jenerali huyo muasi anayeungwa mkono na Saudia, Imarati, Misri na baadhi ya nchi, linajiita Jeshi la Taifa la Libya.
-
Maandamano ya kupinga vita yafanyika mbele ya balozi za Imarati katika nchi za Ulaya
Dec 03, 2019 07:39Wanaharakati wa kutetea haki za binadamu wamefanya maandamano hadi mbele ya balozi za Umoja wa Falme za Kiarabu katika nchi kadhaa za Ulaya.
-
Baraza la Usalama lazionya nchi zinazoendelea kumimina silaha Libya
Dec 03, 2019 07:35Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limetoa onyo kali kwa nchi zinazokiuka azimio la baraza hilo na kuendelea kurundika silaha nchini Libya.
-
Vikosi vya Haftar vyaua raia 14 katika mji mkuu wa Libya, Tripoli
Dec 03, 2019 03:23Kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya linaloongozwa na Khalifa Haftar linatuhumiwa kufanya mashambulizi ya anga katika mji mkuu wa nchi hiyo Tripoli ambayo yameua raia 14.
-
Shehena ya silaha kutoka Imarati yawasili nchini Libya
Nov 29, 2019 11:18Duru za habari nchini Misri zimeelezea kuwasili nchini Libya shehena ya silaha kutoka Imarati.
-
UN yakanusha kuwatendea maovu wahajiri walioko Libya
Nov 29, 2019 07:19Umoja wa Mataifa umekadhibisha ripoti zinazodai kuwa wafanyakazi wa taasisi hiyo ya kimataifa wamewatendea isivyo wahajiri walioko katika kambi za wakimbizi nchini Libya.
-
Wapiganaji wa Haftar watungua drone ya Marekani 'kimakosa'
Nov 26, 2019 04:15Kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya linaloongozwa na Khalifa Haftar limetangaza kuwa lilitungua ndege isiyo na rubani ya Marekani kwa bahati mbaya.
-
Rais wa Chad akosoa vikali uingiliaji wa NATO katika masuala ya ndani ya Libya
Nov 23, 2019 07:56Rais Idriss Deby wa Chad amesisitiza kuwa, uingiliaji wa Shirika la Kijeshi la Nchi za Magharibi (NATO) katika masuala ya ndani ya Libya ulipelekea kutokea maafa katika nchi hiyo na kwamba, Afrika haipaswi kubeba peke yake mzigo wa maafa hayo.
-
Sudan na Chad zapokea makumi ya wahajiri waliotimuliwa Libya
Nov 18, 2019 11:38Serikali ya Libya imewahamishia katika nchi za Sudan na Chad makumi ya wahamiaji haramu.
-
Mjumbe wa UN Libya alikosoa Baraza la Usalama kwa kushindwa kutatua mgogoro wa nchi hiyo
Nov 14, 2019 09:38Mkumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Libya amelikosoa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa kushindwa kuchukua maamuzi kuhusiana na nchi hiyo.