-
Iran yalaani mauaji ya Mmarekani mweusi yaliyofanywa na polisi Los Angeles
Jan 14, 2023 23:59Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali mauaji ya kikatili ya raia wa Marekani mwenye asili ya Afrika, yaliyofanywa na polisi ya nchi hiyo akisisitiza kuwa, Washington inapaswa kubebeshwa dhima ya wimbi la ukatili dhidi ya Wamarekani weusi.
-
Siasa za upande mmoja za Marekani dhidi ya Iran; kudhoofishwa utawala wa sheria na kukiukwa Hati ya Umoja wa Mataifa
Jan 14, 2023 03:32Akizungumza Alkhamisi katika kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kilichofanyika chini ya anwani "Kukuza na Kuboresha Utawala wa Sheria katika Kudumisha Amani na Usalama wa kimataifa" Amir Saeed Iravani, Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika umoja huo amesema kwamba hatua zisizo za kisheria na za upande mmoja za Marekani dhidi ya nchi huru wanachama wa Umoja wa Mataifa, kama vile Iran, zinadhoofisha utawala wa sheria na kukiuka Hati ya umoja huo.
-
Muelekeo wa kiundumakuwili na wenye mgongano wa Marekani kuhusiana na JCPOA
Jan 11, 2023 05:48Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani Ned Price amesema, hatua ya upande mmoja iliyochukuliwa na serikali ya rais wa zamani wa nchi hiyo Donald Trump ya kujitoa kwenye makubaliano ya nyuklia ya JCPOA ni kosa kubwa zaidi la kistratejia lililofanywa katika miaka ya karibuni kwa upande wa sera za nje za Washington.
-
Ubaguzi washadidisha mgogoro wa 'afya ya umma' Marekani
Jan 10, 2023 04:22Miji na kaunti zaidi ya 200 nchini Marekani zimeutangaza ubaguzi wa rangi nchini humo kama mgogoro wa afya ya umma. Wataalamu wa afya wameonya kuwa, ubaguzi wa kimfumo wa miongo kadhaa umeendelea kuathiri afya za Wamarekani wasio wazungu.
-
Maelfu ya wauguzi wafanya mgomo New York, Marekani
Jan 10, 2023 00:14Wauguzi zaidi ya 7,000 katika hospitali mbili kubwa jijini New York nchini Marekani wameanza mgomo baada ya mazungumzo yao na serikali kuhusiana na mazingira yao ya kazi, nyongeza ya mishara na sera za wafanyakazi kugonga mwamba.
-
Mashambulio ya kikatili ya Marekani yaongezeka nchini Somalia
Jan 09, 2023 23:04Tovuti moja ya nchini Marekani imetangaza habari ya kuongezeka mashambulizi ya anga ya Marekani nchini Somalia wakati wa urais wa "Joe Biden" na mauaji ya raia katika nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Sheikh Naim Qassim: Hujuma za kihabari na kigaidi za Marekani dhidi ya Iran zimegonga mwamba
Jan 08, 2023 08:37Naibu Katibu Mkuu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, hujuma za kihabari na kigaidi za Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zilizokuwa zikiendeshwa katika fremu ya machafuko yaliyokuwa yameibuka nchini Iran zimesambaratika na kugonga mwamba.
-
Iran yasisitiza kulipiza kisasi mauaji ya Jenerali Soleimani na kufukuzwa vikosi vya kigaidi vya Marekani
Jan 08, 2023 01:16Mkuu wa Kamandi Kuu ya Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa Iran italipiza kisasi dhidi ya wahusika wa kitendo cha kigaidi cha mauaji ya Luteni Jenerali Soleimani na kusisitiza kuwa "kesi hii itabaki wazi hadi magaidi hao watakapoadhibiwa."
-
Mtoto wa miaka 6 ampiga risasi mwalimu wake kwa 'makusudi' Marekani
Jan 07, 2023 06:38Mtoto wa miaka sita huko nchini Marekani ametiwa mbaroni baada ya kumpiga risasi na kumjeruhi vibaya mwalimu wake katika mji wa Newport News, jimboni Virginia.
-
Ammar Hakim: Kosa la Marekani la kuwauwa makamanda wa muqawama halisameheki
Jan 04, 2023 04:04Sayyid Ammar Hakim, Kiongozi wa Harakati ya Hikma ya Kitaifa ya Iraq amesema kuwa, kosa la Marekani la kuwauwa makamanda wa ushindi wa muqawama halisameheki.