-
Ilhan Omar ataka ufafanuzi wa Biden juu ya shambulio la anga Somalia
Jul 24, 2021 20:50Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi la Marekani kwa tiketi ya chama cha Democratic amemuandikia barua Rais Joe Biden wa nchi hiyo, akitaka ufafanuzi na maelezo kuhusu shambulio la kwanza la anga lililofanywa na utawala wake nchini Somalia.
-
HRW: Biden anapaswa kusitisha uuzaji wa silaha kwa tawala zinazokiuka haki za binadamu
Jul 24, 2021 10:18Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Righs Watch limemtaka Rais Joe Biden wa Marekani asitishe uuzaji wa silaha kwa wakiukaji wa haki za binadamu zikiwemo tawala za Misri na Israel.
-
Muqawama wa Iraq waonya kuweko matokeo mabaya ya kushirikiana kiusalama na Marekani
Jul 24, 2021 03:37Kamati ya Uratibu ya Makundi ya Muqawama ya Iraq imesisitiza juu ya kutoruhusiwa uwepo wa aina yoyote ile wa majeshi ya kigeni katika ardhi ya nchi hiyo ya Kiarabu.
-
HRW yamtaka Biden asitishe uuzaji wa silaha kwa tawala zinazokiuka haki za binadamu
Jul 23, 2021 23:24Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch (HRW) limemtaka Rais Joe Biden wa Marekani kuziwekea vikwazo vya silaha tawala zinazokiuka haki za binadamu
-
WSJ: Marekani kuondoa askari wake Iraq kufikia mwishoni mwa 2021
Jul 23, 2021 03:16Gazeti la Kimarekani la Wall Street Journal limedai kuwa, Marekani na Iraq zimeafikiana juu ya kuondoka wanajeshi wote wa US kutoka katika nchi hiyo ya Kiarabu kufikia mwishoni mwaka huu 2021.
-
Kufichuliwa engo mpya wa ushirikiano wa Marekani na kundi la Daesh nchini Afghanistan
Jul 22, 2021 07:00Zamir Kabulov, mjumbe wa Rais wa Russia katika masuala ya Afghanistan amesema katika mkutano wa Valdai Discussion Club kwamba: Askari wa Marekani na waitifaki wake walikuwa na mawasiliano na ushirikiano na kundi la kigaidi la Daesh nchini Afghanistan.
-
Vifo vya utumiaji wa madawa ya kulevya Marekani vyaongezeka kwa asilimia 30
Jul 18, 2021 06:55Takwimu za vifo vinavyosababishwa na utumiaji wa madawa ya kulevya wa kupindukia nchini Marekani zinazonyesha kuwa, vifo hivyo viliongezeka kwa asilimia 30 mwaka jana (2020) ikilinganishwa na mwaka wa kabla yake yaani 2019.
-
Hizbullah: Marekani ndiye msababishaji mkuu wa masaibu yote ya Lebanon
Jul 17, 2021 03:17Mkuu wa Baraza la Utekelezaji la Hizbullah ya Lebanon amesema, uingiliaji wa Marekani ndio sababu kuu ya masaibu yote ya Lebanon na akasisitiza kwamba, fitna ya Marekani inaandama na kuhujumu kila sehemu ya eneo la Asia Magharibi ulipo muqawama na uteteaji wa sharafu na heshima.
-
Zarif: Marekani inaficha uhalifu wake kwa kuzitupia tuhuma nchi nyingine
Jul 16, 2021 22:40Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amejibu propaganda chafu mpya za Marekani ndhidi ya Iran na kuishauri Washington ishughulikie masuala ya ndani ya nchi hiyo badala ya kuzitupia tuhuma nchi nyingine.
-
Pentagon yakiri: Wauaji wa Rais wa Haiti walikuwa na uhusiano na jeshi la Marekani
Jul 16, 2021 22:39Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani, (Pentagon) amekiri kwamba, wauaji wa Rais wa Haiti walipewa mafunzo na jeshi la nchi hiyo.